Aliegundua madini ya Tanzanite Mzee Jumanne Ngoma Afariki Dunia

Mzee Jumanne Ngoma ambaye aligundua Madini ya Tanzanite amefariki dunia leo January 30, 2019 katika Hospital ya Taifa Muhimbili alipokuwa anapatiwa matibabu.

Akithibitisha kifo cha Mzee Ngoma, Mtoto wake ambaye ni Mtangazaji wa Clouds TV Hassan Ngoma amesema Mzee amefariki leo akiwa anapatiwa matibabu na taratibu za mazishi zitatolewa baada ya kikao cha familia

Aprili 6 mwaka jana, Rais John Magufuli akizindua ukuta wa mgodi wa Tanzanite, Mirerani mkoani Manyara alimzawadia Sh100 milioni kama shukrani kwa mchango wake kwa kugundua madini hayo.



from MPEKUZI

Comments