Riwaya Kali: POWER - Sehemu ya 22


MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA- 0657072588
ILIPOISHIA   

“Nimekuelewa kocha”
“Weweee mimi sio kocha ni kapteni”
Kauli yangu ikawafanya wanafunzi wachezaji wezangu kucheka. Gafla mlango wetu ukafunguliwa na sote tukastuka, akaingia daktari wa timu huku akionekana kujawa na wasiwasi.
“Kuna nini?”
“Njooni kocha amejinyonga”
Kauli ya daktari ikatufanya tutoke humu ndani kwa kasi sana na kikimbilia chumbani kwa kocha, kitendo cha kuingia ndani humu nikajikuta miguu ikiniishia nguvu kabisa kwani ni kweli kocha amejinyonga bafuni kwenye bomba kubwa la maji kwa kutumia tai yake.

ENDELEA
Tukiwa katika hali ya sinto fahamu, akaingia meneja wa hoteli hii huku akiwa ameongozana na baadhi ya wafanyakazi wa kiume. Wakaanza kufanya juhudi za kumtoa kocha kwenye bomba hilo, wakafanikiwa na kumlaza kocha sakafuni, daktari akainama na kuweka sikio lake katika kifua cha kocha, akatutazama.
 
“Bado mapigo yake ya moyo yanadunda”
Daktari alizungumza huku akianza kuminya kifua cha kocha. Wakaingia madaktari wakiwa na machela, wakampakiza kocha juu ya kitanda hicho, wakamfunga mikanda ya kitanda hicho ili asipate mitikisiko. Wakamuwekea mashine maalumu ya kupumulia na kuanza kukisukuma kitanda hicho kuelekea katika lifti za gorofa hili. Mimi na wachezaji wezangu tukaingia kwenye lifti nyingine na tukaanza kuelekea chini. Tukafika chini na kukuta madaktari wakimuingiza kocha kwenye gari la wagonjwa na kuondoka naye katika eneo hili huku gari hiyo ikiwashwa ving’ora vya kuashiria hatari. Gari mbili za polisi zikafika katika eneo hili la hotelini. Wakashuka askari kumi na kuelekea katika chumba ambacho kocha alijinyonga.
“Nani kiongozi wenu hapa”
Mmoja wa askari alizungumza.
“Mimi”       
Nilijibu huku nikimtazama askari huyu usoni mwake na kwa kujiamini.
 
“Unaweza kutuambia ilikuwaje?”
Nikashusha pumzi taratibu ili kuyarudisha mapigo yangu ya moyo kwenye mfumo wake wa kawaida, kwani wasiwasi na woga ndivyo vilikuwa vimenitawala.
“Tulikuwa chumbani kwangu na wachezaji wenzangu, daktari yeye ndio aliye kuja kutuita na kutuambia kwamba kocha amejinyonga”
“Daktari gani?”
“Daktari wetu wa timu”
“Anaitwa nani?”
“Ruben”
Kila nilicho kizungumza askari huyu anakiandika kwenye kijikitabu chake kidogo.
“Daktari yuppo wapi?”
“Amepanda gari la wagonjwa na ameambatana na mgonjwa”
“Sawa, wakusanye wezako ili tuweze kuwahoji mmoja baada ya mwengine?”
 
“Maeleo ambayo wao watakupa ndio niliyo kupa mimi, unavyo hitaji niwakusanye kwa pamoja ni kuzidi kuwapa presha na isitoshe kesho tuna mechi ya kwanza mchana. Sinto penda wachezaji wezangu wazidi kupatwa na presha”
Nilizungumza kwa kujiamini sana hadi askari huyu akanikodolea macho ya mshangao.
“Naomba ufanye hivyo kwa maana ni mahojiano ya kawaida kabisa”
Nikashusha pumzi huku nikitabasamu kidogo, nikaingia chumbani kwangu na bahati nzuri nikawakuta wachezaji wezangu wote. Frenando akanifwata huku mwili mzima ukimtetemeka.
 
“Ethan naogopa”
“Unaogopa nini?”
“Mimi naweza kutiwa hatiani kwa tukio hili?”
“Hakuna kitu kama hicho kwani wewe ndio ulimpa tai ajinyonge?”
Niliendelea kuzungumza kwa kujiamini japo kwa namna moja ama nyingine nami nina wasiwasi mwingi sana na kama ni kweli Frenando atahisiwa juu ya picha za nguno alizo mpiga kocha basi matatizo yanaweza kuwa makubwa sana.
“Futa picha hizo kwenye simu yako na ikiwezekana simu pia iviunje kabisa”
 
Nilizungumza kwa sauti ya chini sana pasipo wachezaji wengine kuweza kusikia na wote kila mmoja yupo katika hali ya majonzi na mashaka.
“Polisi wanahitaji kufanya mahojiano na sisi hivyo naomba mujiandae kila mmoja akajibu kitu sahihi kama atakavyo ulizwa. Mumenielewa?”
Wachezaji wezangu wakaanza kulalama huku wengi wao wakitetemeka. Hali hii ikaniogopesha sana kwa maana kesho ndio siku ambayo tunatakiwa kucheza mechi yetu ya kwanza na hali ndio kama hivi.
“Hei nawaomba mutulie musiwe na wasiwasi wa aina yoyote kila kitu kitakwenda kuwa sawa. Mumenielewa?”
Hapakuwa na mchezaji aliye weza kunijibu, nikafungua mlango na kuwatazama askari watatu ambao wananisubiria mlangoni hapa.
 
“Nitahitaji mutakapo wahoji wachezaji wangu, mimi mwenyewe niwepo?”
“Hilo sio jukumu lako kuwepo, tunacho hitaji ni kuzungumza na wacheji mmoja baada ya mwengine”
“Nimezungumza hivyo nikiwa nina maana kubwa sana na kama mutashindwa kukubaliana nami basi sinto ruhusu mchezaji wangu hata mmoja kuhojiwa na mahijiano mutayafanya pale atakapo kuja mwanasheria wa shule au mwalimu mkuu sawa”
Kujiamini kwangu kidogo kukateteresha msimamo wa hawa maaskari ambao walisha kazana kumuhoji mchezaji mmoja baada ya mwengine.
“Sawa”
“Mahojiano yatafanyika kwenye moja ya chumba ambacho wachezaji wangu wanakaa, tena chumba hicho hapo mbele yangu”
 
Nilizungumza huku nikiwaonyesha chumba kinacho tazamana na chumba changu.
“Tungehiji majina ya wachezaji wako yote”
“Nendeni mapokezi, mutaweza kuona majina hayo”
Majibu yangu dhairi yakaonyesha kuto wapendeza hawa askari. Tukamuona mkuu wa shule na mwanasheria wakifika katika eneo hili. Wakasalimiana na askari hawa na kuanza mazungumzo yao ambayo sikuhitaji kuyasikia kwani ninacho kihitaji hivi sasa ni akili ya vijana wangu kuweza kuwa sawa.
“Jamani mahojiano yamesimama kwa muda, ila nina jambo ninahitaji kuzungumza nawe, naomba tukusanyike”
Wachezaji wezangu wakanitiia na wote wakaanza kukusanyika na kunizunguka.
“Frenando yupo wapi?”
“Bafuni”
“Samahani nisubirini”
 
Nikapita katikati ya wezangu hadi bufani, nikamkuta Frenando akiwa amekaa kwenye sinki huku akilia kwa uchungu sana. Nikamtazama kwa muda kisha nikachuchumaa mbele yake.
“Hei Frenando”
“Mmmm”
“Unalia nini rafiki yangu”
“Ethan ninakwenda jela mimi”
“Nisikilize kitu kinacho itwa jela hivi sasa fanya kukisahau. Kumbuka kwamba hujahusika kwenye jambo la aina yoyote ile. Kumbuka kwamba maamuzi ya kujinyonga ni ya mtu mwenyewe na bahati nzuri kocha hajakufa, na hawezi kukutaja wewe katika hili swala kwamba umehusika na tukio lake. Umenielewa”
Frenando akaka kimya huku akinitazama usoni mwake.
“Pia mimi rafiki yako nina pesa, nitahakikisha hakuna jambo lolote ambalo linaweza kutoka kwenye maisha nakuahidi hivyo”
 
“Kweli Ethan”
“Niamini mimi rafiki yangu, ninaapa kwa jila la mwenyezi Mungu siwezi kukuacha upate matatizo.”
Frenando akanikumbatia kwa furaha sana huku akijipangusa machozi usoni mwake.
“Njoo tuwape wezetu mioyo ya kucheza mechi ya kesho. Ukiwa na huzuni wewe unahisi mimi nitafanya nini kwa hawa wachezaji. Tafadhali Frenando”
“Sawa kaka nimekuelewa”
Frenando akasimama nami nikasimama, tukakumbatia kwa sekunde kadhaa.
“Ulifuta zile picha?”
“Ndio na simu nimeivunja vunja na kuidumbukiza huku chooni”
“Sawa”
 
Tukatoka chumbani humu na kumkuta mkuu wa shule akizungumz ana wachezaji. Tukajisogeza katika eneo hilo.
“Kocha wenu ndio kama hivyo amepata matatizo hakuna haja ya kuendelea kuwemo katia mashindano haya ni vyema tukakubaliana kwa pamoja, mujitoe na mutashiriki mwakani. Hali zenu hapa wote mumejawa na wasiwasi mwingi sana. Ili kuto itia shule na taifa aibu basi ni vyema musishiriki”
Maneno ya mkuu wa shule yakanikere sana na kujikuta nikikatiza katikati ya wachezaji wezangu na kusimama mbele yake.
“Kwani kocha ndio anacheza uwanjani?”
Nilimuuliza mwalimu mkuu huku nikimkazia macho.
“Kocha ndio kiongozi wa timu sasa nyinyi kama nyinyi mutafanya nini?”
“Mkuu nakuomba katika timu yangu usiweze kuendelea kuzungumza ujinga na upuuzi wa kuwakatisha tamaa wachezaji wangu. Rudisha tumbo lako shuleni kule ukakae na walimu wezako mkacheke cheke. Sawa”
 
Mwalimu mkuu akanitazama kwa hasira kwani maneno niliyo yazungumza yana udhalilishaji ndani yake kwani ana kitambi kikubwa.
“Niachie timu hii nitaiongoza mimi mwenyewe na nitahakikisha kwamba siku moja inaweka heshima katika nchi hii na dunia. Huna taaluma ya kuongoza mpira sawa”
“Ethan tazama kinywa chako”
“Siwezi kutazama kinywa changu kwa ujinga na uzembe unao zungumza. Mimi hapa ni timu kampteni na sio mwalimu mkuu na sizungumzi kama Ethan, nazungumza kama kiongozi wa wezangu. Kama wao wamekuogopa kuzungumza kile wanacho kihisi katika mioyo yao, basi mimi nitakuambia ukweli kwanza ninakuomba uweze kutoka humu ndani”
 
“Unanifukuza?”
“Sikufukuzi, ila hatukuhitaji humu ndani”
“Sasa ninapiga simu kwa waandaaji wa hii michezo na ninawambia timu yangu inajitoa na wachezaji wangu haw…….”
Kabla ya mwalimu mkuu kumaliza kuzungumza jambo lolote nikajikuta nikimkaba kooni mwake na kumsukomia hadi ukutani na kumkazia machohuku nikiendelea kumtazama kwa hasira sana hadi wachezaji wezangu wakashangaa.
“Kwenye maisha yangu sipendi kuyumbishwa, sipendi mwanaume asiye jiamini kwa maamuzi yake. Uliamua timu ije kwenye michuano na si timu ije kuyumbishwa na mpuuzi mwenzako aliye jinyonga na kuanzia hivi sasa hatuhitaji kocha wa aina yoyote. Nitasimama kama kocha mchezaji umenielewa?”
 
Nilizunugmza huku nikiendelea kumkaba mwalimu mkuu koo lake, akatingisha kichwa akimaanisha kwamba amenielwa, nikamuachia taratibu na kumfanya anza kukohoa sana huku akihema kwani kama ningeongeza dakika mbili katika kumkaba koo lake basi angepoteza maisha.
“Potea ndani ya chumba chetu”
Mwalimu mkuu akatia amri niliyo muamuru na akatoka chumbani kwangu na kuwafanya wachezaji wangu wote kupiga makofi.
 
“Hatuwezi kuyumbishwa, sisi ni wanaume na hakuna mwanamke humu ndani, hakuna mseng** humu ndani. Tukiachana na swala zima la kuleta heshima ya shule, ila tucheze kwa ajili ya heshima zetu sisi wenyewe. Kesho na kesho kutwa tutajenga historia yetu sisi wenyewe. Historia ambayo haito jengwa na mwalimu mkuu, bali ni kwa juhudi zetu sisi wenyewe. Mawazo juu ya kocha yapotee, tufikirie mechi ya kesho na hata kocha msaidizi akifika kesho alfajiri hakuna haja ya kumpa nafasi ya kuvuruga kile tulicho kipanga. Mumenielewa?”
“Tumekuelewa kiongozi”
Nikanyoosha mkono wangu wa kulia katikati ya duara hili tulilo zunguka na kila mchezaji akanyoosha mkono wake na tukaiweka kwa pamoja ikiwa ni ishara ya mshikamano wetu na umoja wetu.
“Mechi ya kwanza hadi ya mwisho, tuhakikishe kwamba tunachezwa kwa ajili ya kuchukua kombe. Kila mmoja acheze kwa uwezo wake wote anao jua yeye. Siku moja mutanikumbuka mukiwa katika klabu kubwa za mpira. Hakuna siri ya mafanikio kama kujituma kwa juhudi pasiopo kukata tamaa. Mumenielewa?”
 
“Tumekuelewa kapteni”
Tukaachanisha mikono yetu. Nikawaruhusu wachezaji wote kwenda kulala. Nikajaribu kumpigia Camila ila nikakuta simu haipatikani.
“Hivi kocha alikuwa anafikiria nini hadi kujinyonga?”
Frenando aliniuliza huku akiwa amelala kwenye kitanda chake.
“Sifahamu kwa kweli. Ila kuna mambo yake mengine aliniambia kwamba anayatafajari, nahisi hayo ndio yamempekekea kuwa katika hali aliyo kuwa nayo”
“Mmmm, Mungu amsaidie apote tu”
“Ni kweli”
“Poa Ethan usiku mwema”
“Nawe pia ndugu yangu”
Nikajifunika shuka langu na kulala usingizi fofofo.
                                                                                                                     ***
Muda wa kueleka katika uwanja ambao ndio zinafanyika sherehe za ufunguzi wa mashindano ya kombe la bara la Ulaya kwa shule za sekondari. Kila mchezaji akabeba kifaa chake anacho hitaji kwenda kukitumia uwanjani.
“Ethan nakuomba”
Koch msaidizi aliniita kabla ya kuingia ndani ya basi. Tukasimama pembeni ya basi hili na kuwaacha wachezaji wengine waendelea kuingia ndani ya basi.
“Ndio kocha”
“Mfumo ambao umekubaliana na wezako kweli mutaweza kuuhimili uwanjani kwa maana timu munayo kwenda kukuata nayo inacheza mfumo wenu?”
Kabla sijamjibu kocha simu yake ikaingia meseji. Nikaa kimya huku nikimtazama kocha anavyo soma meseji hiyo. Akashusha pumzi huku akinikabidhi simu simu yake ili niisome meseji hiyo.
 
‘Shule haito husika kwa chochote kwenye swala la mshahara wako wa ukocha, malezi na matumizi ya timu yako la sivyo jiudhuru ukocha tumuachie huyu mpumbavu timu tuoneka kama ataweza kuiongoza. Bili ya hotelini, leo ndio itakuwa siku yenu ya mwisho kukaa, nimeisitisha na muthithubutu kurudisha miguu yenu kwenye hiyo hoteli sawa Robert’
“Kocha ni nani huyu?”
“Mwalimu mkuu wenu”
Nikajikuta nikiachia msunyo mkali sana kwani sijui ni kitu gani mwalimu mkuu huyu anakifikiria kwenye ufahamu wake wa akili hadi kuamua kumshinikiza kocha kuacha ufundishaji wa timu hii.

==>>ITAENDELEA KESHO


from MPEKUZI

Comments