Riwaya Kali: POWER - Sehemu ya 21

MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA- 0657072588
ILIPOISHIA   
   “Usiseme Ethan kocha. Tambua nimebeba dhambi kubwa sana ya kumdanganya mke wako. Je dhambi hiyo mimi nina ilipaje eheee?”
“Ethan natambua nyinyi bado ni wadogo, ila muikingia kwenye ndoa mutaweza kujua ni nini kinacho tokea hadi wanaume tunaamua kuwa na wake wa nje”
“Wacha weeee”
Frenando alizungumza kwa kejeli huku akimtazama kocha usoni mwake. Gafla simu yangu ikaanza kuita ikiwa ndani ya kibegi changu mgongoni. Kocha akatoka na macho ya hasira kwani moja ya sheria tukiwa kambini ama shuleni haturuhusiwi kuwa na simu.
“Ethan kwa nini una simu?”
Kocha aliniulza kwa kunifoke sana.
“Acha upuuzi wewe mzee. Muache apokee simu la sivyo tunakwenda kuzungumza uchafu wote kwa mke wako na ushahidi wapicha ninao”
Frenando alizungumza kwa kujiamini na kumfanya kocha kumkodolea macho na kukosa jambo la kuzungumza kwa muda huu.

ENDELEA
Nikamtazama kocha kwa muda kisha nikachukua simu yangu ndani ya kibegi na kukuta ni namba kutoka nchini Tanzania. Nikaipokea kwa haraka na kuiweka sikioni mwangu.
“Haloo”
“Ethan”
 
“Niambie mke wangu”
Nilizungumza huku nikiwa nimejawa na furaha sana huku nikiondoka katika eneo hili na kumuacha Frenando na kocha.
“Safi Ethan wangu, samahani sana kwa kushindwa kuweza kuzungumza nawe mpenzi wangu baada ya kufika”
“Usijali mpenzi wangu, ila si mumefika salama?”
“Ndio tumefika salama na asubuhi ya leo tutaanza rasmi ziara yetu ya kimasomo”
“Sawa mpenzi wangu ila ninahitaji nikuombe kitu kimoja”
“Kitu gani tena mpenzi wangu?”
“Utanikubalia?”
“Ndio mpenzi wangu nitakukubalia wewe ni mume wangu lazima ninacho kuomba niweze kukubalia.”
“Ni jambo gumu lakini”
“Niambie tu Ethan, kumbuka mimi nipo kwa ajili yako mume wangu”
“Nakuomba mukimaliza ziara yenu nchini Tanzania, usiende nchini Somalia”
“Kwa nini?”
 
“Nahisi kuna hali ya hatari itakwenda kuwatokea huko mpenzi wangu”
“Usijali mume wangu, hapa nilipo tu kuna walinzi walitangulia wiki moja kabla ya kuja nchini hapa Tanzania kwa ajilli ya kunilinda na hata huko Somalia walisha tangulia walinzi kama mia moja hivi. Wapo kwa akili yangu mume wangu”
Camila alizungumza kwa kujiamini sana na kunifanya nishushe pumzi taratibu huku nikifikiria cha kumuambia.
“Usiwe na wasiwasi Ethan wangu, tamua nina lindwa sana na hakuna wa kuniletea ubaya wa aina yoyote sawa mume wangu”
“Sawa ila nakuomba ikiwezekana usiende”
“Usijali nitakuwa nikikujulisha kwa kila hatua ambayo nina fikia”
“Sawa mke wangu”
“Ngoja nijiandae kesho nitakupigia mchana tukiwa tuna rudi”
“Sawa sawa”
 
Camila akakata simu na taratibu nikashusha pumzi na kurudi alipo simama Frenando.
“Mzee wako anatetemeka, amesha ingia ndani ya gari”
“Kwani ushahidi wa picha unao kweli au?”
“Ndio cheki hizi hapa”
Frenando akanionyesha picha za kocha na muhudumu wa hoteli jambo lililo ishangaza sana.
“Umezipiga piga vipi?”
“Muda ule nilivyo mrudishia simu, niliingia kwa kunyata ndani kwao papiso wao kujijua kwani walikuwa wapo katikati ya dimbwi la mapenzi basi nikawapiga picha za kutosha kisha nikawastua”
Tulizungumza huku tukiingia kwenye basi la wachezaji wezetu. Safari ya kurudi hotelini ikaanza taratibu huku kocha wetu akiwa amekaa siti ya mbele kabisa akionekana sio mtu mwenye furaha kabisa.
“Frenando futa hizo picha”
“Kwa nini?”
 
“Isije baadae zikaleta matatizo si unajua tupo kwenye kipindi cha mashindano na mwalimu anahitaji furaha na akili yake iweze kutulia ili aweze kufanya kazi yake kwa umakini”
“Sasa Ethan unahisi huyu katika makocha kweli ni kocha. Tunacho kifanya uwanjani ni juhudi zetu tu. Acha kwanza tumpe tumbo joto akipata akili basi atanitafuta na kukaa nami kwa upole na kuniomba msamaha”
“Msamaha wa nini tena?”
“Si unamfahamu yule mwanaye wa kike?”
“Ndio”
“Mzee alinichimba biti siku moja, sikutaka kukuambia tu. Akaniahidi akiniona naye atanipiga risasi”
“Weee”
“Ndio hataki niwe mkwe wake”
“Ila vipi mwanaye anakupenda?”
“Ndio ananipenda, na hata yeye anajisikia vibaya sana juu ya baba yake kutukataza kuwa katika mahusiano”
“Duuu”
 
“Yaa mzee analeta swaga eti mimi Mmexco siwezi kumuoa Mjerumani”
“Ana wazimu, kwa hiyo mimi Mtanzania nisioe Mjerumani?”
“Ndio maana yake”
“Poa endelea kuzishikilia ila hakikisha kwamba simu yako hupotezi wala hakuna mtu mwengine wa kuziona”
“Poa poa”
Tukafika hotelini, tukaingia kwenye vyumba vyetu vya kulala. Tukaoga kisha tukaijiandaa kwa chakula cha usiku, ambacho tunakula kwa pamoja na siku inayo fwata tunaanza mechi yetu ya kwanza. Tukiwa katika eneo la chakula, kocha hakuwa na furaha kabisa. Hata mipango ya kupanga kesho tucheze mfumo gani kocha hazungumza kabisa jambo ambalo lilianza kuwashangaza hadi wachezaji wengine kwani si kawaida yake, kwani katika kipindi cha nyuma huwa hutumia muda wa chakula kuweza kupanga mipango na sisi wachezaji wake.
 
“Ethan”
“Mmmm”
“Hembu mfwate kocha kwa maana anaonekana hayupo sawa”
Mchezaji mmoja aliniambia kwa upole huku akinitazama usoni mwangu.
“Sawa”
“Tunakutegemea Ethan kumbuka wewe ndio timu kapteni”
Nikanyanyuka na kumfwata kocha alipo kaa, nikavuta kiti cha pembeni na kukaa huku nikimtazama usoni mwake.
“Kocha kuna tatizo gani?”
Kocha akanitazama kwa muda kisha akashusha pumzi nyingi.
“Kuna mambo ninatafakari”
“Mambo gani kocha, unaweza kunishirikisha”
Kocha akaingiza mkono mfukoni na kutoa karatasi nyeupe na kunikabdhi. Akanyanyuka kwenye kiti alicho kikalia na kunitazama.
“Hakikisha unawapa maelekezo wezako juu ya mchezo wa kesho”
 
Kocha baada ya kuzungumza hivyo akaondoka na kuniacha nikimsindikiza kwa macho. Nikafungua karatasi hii na kuoona ikiwa imeandikwa mfumo wa jinsi gani tunavyo takiwa kucheza kesho nani aanze na nani apumzike. Nikaikunja vizuri karatasi hii na kuiweka mfukoni mwangu.
“Mukimaliza kula tukutane chumbani kwangu wote”
“Sawa”
Wachezaji waliitikia kwa pamoja huku wakionekana kujawa na furaha.
“Dokta hembu kazungumze na kocha tujue ana sumbuliwa na nini?”
“Alisha nieleza anahitaji muda wa kupumzika kidogo ndio maana nilimuacha akae peke yake”
Kocha wa timu alinijibu huku akinitazama usoni mwangu.
“Kocha msaidizi anakuja lini?”
“Kesho asubuhi”
“Sawa”
Nikamfwata Frenando alipo kaa.
“Mzee sijui ni wewe ndio umemchanganya?”
“Kivipi?”
 
“Si umemuona leo alivyo nyeshewa na mvua”
“Ohoo pale nahisi anafikiria juu ya makubaliano tuliyo wekeana”
“Yapi tena?”
“Mara moja hii umesha sahau”
“Niambie”
“Nimemuambia, anipe mwanaye kiroho safi nami nifute picha hizi la sivyo tuna haribiana”
“Hiyo unahisi ni njia sahihi ya kuanzisha mahusiano na baba mkwe wako?”
“Ethan kuna njia gani nyingine zaidi ya hiyo. Mimi nimejitahidi kadri ya uwezo wangu kuhakikisha kwamba mzee ananikubali, ila wapi. Hata golini ninavyo jituma nisifungwe magoli, si kwamba ni kwaajili ya timu hapana. Nikwaajili yake, ili aone kwamba mkwe wake nina muhitaji mwanaye ila ananiletea upuuzi tu”
 
Frenando alizungumza kwa msisitizo mkali huku akinitazama usoni mwangu.
“Achagua moja tu, mtoto kunikabidhi au nizimwage kwenye mtandao na ikitokea nimeziachia kwenye mtandao basi ukocha anapoteza, ndoa inakufa. Hata huyo mwanaye anaye hisi kunibania pia atamkosa na kiulaini nitamchukua mwanaye”
Nikamtazama Frenando kwa muda kidogo jinsi anavyo ipanga mipango yake, nikajikuta nikicheka mwenyewe.
“Nini kinacho kuchekesha?”
“Mipango unayo ipanga ni ya mbali sana pasipo kufikiria madhara kwa upande wako”
“Upande wangu madhara yake yapo vipi?”
“Tambua akiamua kukufungulia hatua za kisheria anaweza kukufunga”
 
“Wapi, ana ushahidi gani kwamba mimi ndio nimefanya tukio hilo na akitaka kunistaki usihisi kwamba nitabaki mwenyewe”
“Una maana gani?”
“Wewe ni rafiki yangu naamini watakuchunguza na wewe wakiamini huu ni mpango wetu sisi wawili, ila ni wangu mimi kama mimi. Natambua kwamba wewe una makampuni mengi sana, sasa hii inaweza kuleta skendo kubwa kama mmiliki wa makampuni amehusika kwenye urushaji wa picha za nguno mtandaoni”
Maneno ya Frenando kidogo yakanistua sana na kunikasirisha kwa kiasi ila nikajaribu kuizuia hasira yangu kwa kutabasamu huku nikimtazama usoni mwake.
“Nakutania bwana Ethan, siwezi kukuhusisha katika maswala yangu haya ya kipuuzi. Kumbuka mama yako ni waziri mkuu Mexco hata likitokea la kutokea, kesi itakwenda kufunguliwa Mexco na si hapa”
“Sawa, maliza kula twende chumbani”
“Sawa kapteni”
 
Nilipo hakikisha kwamba wachezaji wezangu wote wamepata chakula, tukaelekea chumbani kwangu. Kutokana vyumba vyetu ni vikubwa, wachezaji wote waliweza kuenea ndani ya chumba hichi.
“Habari zenu”
“Safi kapteni”
“Kesho ndio tunaanza michuano yetu rasmi. Tukumbuke kwamba tuna maadui wengi sana kwenye haya mashindano. Maadui ambao wapo tayari kuhakikisha kwamba timu yetu inatoka mapema sana kadri wao wanavyo amani.”
“Ushikamano wetu, muunganiko wetu. Ujasiri wetu na kujituma kwetu ndio misingi kamili ya kuwaangusha maadui. Tumezoeleka kuwa na mifumo minne ya kimichezo. Mifumo ambayo makocha wengine wa timu nyingine ni lazima watakuwa wamesha ifanyia kazi na kujua ni nani na nani ambaye atakabwa ili timu isitembee”
 
Nilizungumza kwa upole huku wachezaji wezangu wote wakinisikiliza kwa umakini sana. Nikatoa karatasi ambayo alinikabidhi kocha nikaifungua mbele yao na kumkabidhi mmoja wao ili atazame nini kilicho andikwa na kocha kisha amkabidhi na mwenzake.
“Tutazame haraka haraka hiyo mifumo ndugu zangu”
Karatasi hiyo ikaendelea kupita kwa kila mchezaji na hadi mwisho ikarudi kwangu.
“Mfumo huo alio panga kocha, unafahamika sana kwa kila mmoja wetu. Pia kwa wachezaji wa timu pinzani. Jambo ambalo litatusababishia kutumia nguvu nyingi sana katika kutafuta magoli na inawezekana pia tukashindwa kupata magoli.”
 
“Ninahitaji mfumo ubadilike. Sisi sote humu ndani kila mmoja anaweza kucheza nafasi zaidi ya mbili si ndio?”
“Ndio”
“Tuachane na mfumo wa 4, 4,2 tucheze mfumo wa 4,3,1,2”
“Mchezo huu utawawezesha viungo kumpa mipira Lukas. Lukasi utasimama hapo kwenye moja, na kutokana una nguvu, kasi na unaweza kukaa na mpira muda mrefu, kazi yangu mimi na Pilo itakuwa ni kupokea mipira kutoka kwako na mipira usiilete kwa njia ya pasi za chini, wataizuia sana. Ilete kwa pasi za juu. Mimi ninaweza kuruka na kuichukua hata Pinto ni hivyo hivyo. Mabeki naamini munafahamu kazi yenu. Apite mtu mpira ubaki au upite mpira mtu abaki. Nyinyi viongo wa katikati, kazi yenu ni kuhakikisha Lukas anakuwa huru, kabeni watu wasielekee kwa mabeki. Kipa, sina wasiwasi na Frenando. Mumenielewa jamani”
 
“Ndio kapteni”
Wachezaji wezangu wakapiga makofi wakionyesha kukubaliana nami katika hili nilio waambia.
“Mwenye swali?”           
“Kampteni je mfumo huu ukituwia ugumu tunafanyaje?”
“Tutakuwa tunabadilisha mifimo ya uchezaji kila baaada ya dakika kumi. Tuanze na mfumo wa kawaida wa 4,4,2 kisha tutabadilika kadri mchezo unavyo zidi kwenda. Kikubwa ninacho kitegemea ni kasi, na Pinto yake mambo yako ya ubishoo wa kupiga chenga ukiwa golini ukitegemea penati sitaki kuyaona. Ukifika golini piga shuti golini, na kipa atajuana yeye mwenyewe na mpira wake. Sijui umenielewa Pinto?”
 
“Nimekuelewa kocha”
“Weweee mimi sio kocha ni kapteni”
Kauli yangu ikawafanya wanafunzi wachezaji wezangu kucheka. Gafla mlango wetu ukafunguliwa na sote tukastuka, akaingia daktari wa timu huku akionekana kujawa na wasiwasi.
“Kuna nini?”
“Njooni kocha amejinyonga”
Kauli ya daktari ikatufanya tutoke humu ndani kwa kasi sana na kikimbilia chumbani kwa kocha, kitendo cha kuingia ndani humu nikajikuta miguu ikiniishia nguvu kabisa kwani ni kweli kocha amejinyonga bafuni kwenye bomba kubwa la maji kwa kutumia tai yake.

==>>ITAENDELEA KESHO


from MPEKUZI

Comments