Breaking News: Rais Magufuli Kaagiza Bendera ya Taifa Kupepea Nusu Mlingoti kwa Siku 3 Kufuatia Ajali ya MV Nyerere

Rais John Magufuli ameagiza Bendera ya Taifa kupepea kwa nusu mlingoti kwa siku tatu kuanzia kesho Septemba 22 kufuatia ajali ya kivuko cha MV Nyerere iliyotokea jana mkoani Mwanza. 

Kauli hiyo ya Rais Magufuli imetolewa na na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi, Dodoma leo  Septemba 21, 2018. 

Amesema Serikali inatoa pole kwa ndugu, jamaa na marafiki wa ndugu waliofarii katika ajali ya MV Nyerere na kuwatakia majeruhi wapone haraka.

Pia Rais Magufuli ameagiza viongozi wa taasisi na mamlaka zinazosimamia usafiri wa majini wahojiwe na watakaobainika kuhusika kwa uzembe wachukuliwe hatua kali

Hadi sasa watu waliothibitika kufariki ni 131.


from MPEKUZI

Comments