BREAKING: CHADEMA Wapata Pigo, Mbunge wa Serengeti Ajiuzulu na Kuhamia CCM

Usiku wa  kuamkia Leo, Septemba 28 Chama Cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA kimepata pigo baada ya kuondokewa na Mbunge wa Serengeti mkoa wa Mara Marwa Chacha ambaye amejiuzulu nafasi yake ya Ubunge na kuhama CHADEMA kisha kujiunga na CCM kwa madai ya kuamua kuunga jitihada za Rais Dr John Pombe Magufuli.

Amesema wakati akigombea ubunge  aliahidi kuwaletea maendeleo wananchi wake lakini dhamira yake haijafanikiwa kutoka na vikwazo anavyokumbana navyo ndani ya Chadema.

Chacha amewataka wakazi wa Serengeti kumchagua mtu atakayeweza kushirikiana nao pamoja ili kuleta maendeleo kupitia CCM


from MPEKUZI

Comments