Mtanzania ala shavu la kuwa miongoni mwa Blogers 50 duniani walioalikwa na Russia, World Cup

Krantz akikabidhiwa bendera na Mkurungezi Mtendaji wa Bodi ya Utalii Tanzania, Devotha Mdachi. 

 *************
 Mwanablogu kutoka Tanzania Krantz Mwantepele kutoka blog ya Mwanaharakati Mzalendo amechaguliwa na serikali ya Russia kuwa miongoni mwa Blogers na social media influencers 50 dunia nzima kwaajili ya kutembelea nchi hiyo kabla michuano hiyo haijaanza mapema Juni 14.
 
Mtanzania huyo pamoja na wenzake atapata fursa ya kutembelea viwanja vyote 5 ambavyo ni Krestovsky Stadim, Fisht Olympic Stadium, Cosco Arena, pamona na Ekaterinburg Arena.z

Krantz ambaye pia ni Katibu wa Tanzania Bloggers Network (TBN), alisema yeye aliomba nafasi hiyo kupitia mitandao ya kijamii baada ya kutumiwa link za marafiki zake.
 
“Nafurahi kuwa mmoja ya Blogers na social media influencers 50 dunia nzima kualikwa na serikali ya Urusi kufanya Coverage ya kombe la dunia na vivutio mbali mbali vya nchini humo,” alisema Krant.
Aliongeza, “Nitakuwa balozi mzuri pia wa utalii wa hapa nchini kwa udhamini mkubwa wa Wonderfultanzania, Nitawakilisha vizuri huko ughaibuni Endelea kufuatilia na koncept_tv na Mwanaharakati Mzalendo Blog nitakupa exclusive zote kupitia huko,”
 
Mwanabloger huyo pia alipongezwa na wadau mbalimbali ikiwemo serikali pamoja na kukabidhiwa bendera ya Tanzania na Mkurungezi Mtendaji wa Bodi ya Utalii Tanzania, Devotha Mdachi.



from MPEKUZI

Comments