Marais wa Korea Kaskazini na kusini wakutana kwa dharula

Viongozi wa Korea Kaskazini na Korea Kusini wamekutana eneo lenye ulinzi mkali kati ya nchi hizo mbili na kufanya mazungumzo ya siri.

Mkutano huo ni wa pili kufanyika kati ya viongozi hao kati ya rais wa Korea Kusini, Moon Jae-in na kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong-un.

Aidha, mkutano huo unafanyika wakati pande hizo zinaendelea na jitihada za kufanikisha mkutano wa kihistoria kati ya Korea Kaskazini na Marekani.

Alhamisi Rais wa Marekani, Donald Trump alifuta mkutano uliopangwa kufanyika tarehe 12 mwezi Juni lakini baadaye akasema kuwa unaweza kufanyika,

Hata hivyo, mazungumzo kati ya Trump na Kim kama yatafanyika huku yatajikita zaidi katika kuondolewa silaha za nyuklia kutoka rasi ya Korea na kumaliza misukosuko.


from MPEKUZI

Comments