Baada Ya Diamond, Lynn Ahamishia Majeshi Yake Kwa Chris Brown

Video vixen Irene Hillary maarufu kama Lynn aliyejizolea umaarufu Kupitia video ya Rayvanny ya wimbo wa ‘Kwetu’ amefunguka kuhusu mahaba mazito kwa supastaa wa kimataifa

Lynn alipata umaarufu baada ya kudaiwa kutoka kimapenzi na staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz hadi kubeba mimba yake.

Lakini hivi sasa Lynn ameweka wazi kuwa mapenzi yake yote yamehamia kwa staa wa Muziki kutoka Marekani Chris Brown na kusema Staa Huyo anamkosesha usingizi akimuwaza.

Kwenye mahojiano na Risasi Jumamosi, Lynn alisema kuwa ametokea kumpenda sana mwanamuziki huyo kiasi ambacho haelewi atafanyaje ila anaomba katika maisha yake siku moja akutane naye, amueleze hisia zake.

“Hivi ulishawahi kumpenda mtu mpaka ukawa huelewi sababu? Sasa ndio mimi nilivyo kwa Chris, naamini siku nitaonana naye na kama ikitokea hivyo kwa kweli nitamfikishia hisia zangu, kama atakubali au kukataa, niwe tu nimemuambia, naamini nitakuwa na amani”.


from MPEKUZI

Comments