Mbunge Awavaa Walimu Wanaofelisha Wanafunzi kwa Rushwa ya Ngono

Mbunge wa Ulanga Goodluck Mlinga amelitaarifu bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, juu ya vitendo vinavyofanywa na baadhi ya walimu wa vyuo vikuu hapa nchini, vya kufelisha wanafunzi wa kike kwa makusudi.

Akichangia hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu na , Goodluck Mlinga amesema walimu hao ambao wanajifanya ni vidume vya mbegu, hufelisha wanafunzi wa kike ili wawape rushwa ya ngono, kuweza kuwawekea maksi za ufaulu.

“Kumekuwa na tatizo la vyo vikuu, wanafunzi wetu wa kike wanapata shida mno, katika vyuo vyetu vikuu kuna walimu wanajulikana kabisa kuwa hawa walimu ni madume ya mbegu, wanafelisha wanafunzi wa kike, wanataka wawape rushwa za mapenzi ndio wawafaulishe”, amesema Goodluck Mlinga

Pia Mheshimiwa Mlinga amesema yupo tayari kupeleka majina ya walimu hao ambao wapo vyuo vyote nchini kwa Waziri wa Elimu, ili waweze kuchukuliwa hatua stahiki.

“Mheshimiwa Waziri nitashirikiana na wewe kama utapenda unipe ushirikiano, nitakuletea majina ya vyuo vikuu vyote Tanzania, ya walimu ambao madume ya mbegu kazi yao ni kufelisha wanafunzi na kutaka rushwa za ngono”, amesema Mheshimiwa Mlinga.


from MPEKUZI

Comments