Hali ya Usalama Iringa Iko Shwari.....Diwani mmoja Katiwa Mbaroni

Hali ya usalama mkoani Iringa leo imeendelea kuwa shwari licha ya tishio la maandamano yaliyotarajiwa kuwepo huku ulinzi ukiimarishwa katika baadhi ya maeneo yenye mkusanyiko mikubwa kama benki na vyuo vikuu.

Hata hivyo, Jeshi la Polisi mkoani hapa linamshikilia kwa mahojiano Diwani wa Kata ya Igumbiro, Musa Mlawa kwa kosa la kufanya mkusanyiko usio halali.

Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa, Juma Bwire Diwani huyo anashikiliwa kwa mahojiano ili kubaini chanzo cha mkusanyiko huo.

Ulinzi mkubwa ulionekana kuimarishwa sana katika lango la kuingilia Chuo cha Kikatoliki ha Ruaha (RUCU) ambacho kinapakana na Benki ya NMB Tawi la Mkwawa.

Katika Chuo Kikuu cha Tumaini Iringa na Chuo cha Elimu Mkwawa hali ilikuwa shwari na ilionekana gari moja tu ikipiga doria ikiwa na askari wachache ikizunguka maeneo tofauti tofauti ya mji wa Iringa.


from MPEKUZI

Comments