Ajali ya Polisi na wanajeshi yauwa Morogoro

Mwanajeshi mmoja wa JWTZ pamoja na mtoto wa Mwanajeshi mwenzake wanadaiwa kupoteza maisha katika ajali iliyohusisha gari la Polisi aina ya Basi lililogongana na gari dogo aina ya Noah iliyokuwa imebeba Wanajeshi wa JWTZ, maeneo ya Bwawani Morogoro

Inadaiwa basi hilo la Polisi lilikuwa likitokea Dodoma huku Noah hiyo iliyokuwa imebeba Wanajeshi takribani 6 pamoja na mtoto wa Wanajeshi mwezao ilikuwa ikitokea Morogoro.

Kamanda wa Polisi wa mkoa wa Morogoro, Ulrich Matei amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo ingawa amekiri kutokuwa na taarifa za undani zaidi kwa sasa




from MPEKUZI

Comments