TANGA RAHA- Sehemu ya Arobaini na Mbili ( 42 )

 AGE………………18+
WRITER…………EDDAZARIA G.MSULWA
ILIPOISHIA

Akanipiga kofi jengine huku akiniporomoshea matusi mengi,akaendelea kufanya anacho kifanya akaanza kuufungua mkanda wa suruali yangu,kabla hajamaliza nikstukia kuona jitu jengine kubwa na lakutisha,lenye mabawa likisimama mbele ya gari letu na kusababisha kishindo kikubwa hadi gari ikatingishika

ENDELEA
Rahma akaniacha na nikamsukumia kwenye siti yake na tukabaki tukiwa tumetazamana na jitu hili ambalo linatisha kupita maelezo.Rahma kwa haraka akawasha gari na kuaanza kuirudisha nyuma kwa mwendo wa kasi,Cha kushangaza jitu hili halikuwa na habari na sisi zaidi ya kubaki likitutuzama.

“Tunaelekea wapi?” Nilimuuliza Rahma
“Hata mimi sijui”
“Twende kwenu”
“Kwetu!!?”
“Ndio kuna kazi nataka kwenda kuifanya”
“Kazi gani?”
“Wewe twende,utaiona huko huko”
Tulizungumza huku Rahma akiendelea kuongeza mwendo wa gari,Tukafika nyumbani kwao na kukuta geti likiwa wazi,Tukashuka ndani ya gari na kujibanza pembezoni mwa geti huku tulichungulia ndani kuangalia kama kuna hali yoyote ya watu kuwemo.Giza zito lililopo kwenye jumba la kina Rahma ikazidi kutopa hofo,Nikatangulia mbele huku Rahma akinifwata nyuma.Tukaingia ndani sote tukiwa makini,Hali ya kuzizima ndani ya nyumba ya kina Rahma ikatufanya tushindwe hata kuwasha taa,mwanga hafifu wa mbalamwezi unao pita kwenye madirisha makubwa ya kioo,unatusaidi kuona vitu vilivyomo ndani ya sable.

“Kipo wapi chumba cha kuhifadhia vitabu?”
Nilizungumza kwa sauti ya chini ya kumnong’oneza Rahma ambaya alinitazama kwa mshangao
“Eddy,umejuaje kwetu kuna chumba cha kuhifadhia vitabu?”
“Rahma hilo sio jibu ninalo litaka mimi.Wewe niambie ni wapi kilipo”
“Twende”
Tukapandisha ngazi za gorofani taratibu huku sote tukiwa makini sana.Tukaingia kwenye moja ya chumba kimoja na kukuta vitabu vingi vikiwa vimepangwa kwenye mbao zilizo pangiliwa vizuri ukutani,Nikabaki nikiwa nimeshika kiuno kwani sikujua ni wapi nianzie hii ni kutokana na wingi wa vitabu uliopo katika chumba hichi kikubwa

 


from MPEKUZI

Comments