Shahidi: Wema Sepetu Alinambia anavuta Bangi kwa starehe

Mahakama  ya Hakimu Mkazi Kisutu imeendelea na kesi inayomkabili muigizaji Wema Sepetu ambapo Ofisa wa Polisi WP Mary ameieleza mahakama kuwa mnamo Februari 4, 2017 Wema alimwambia anatumia bangi kwa ajili ya starehe na si kuuza

WP Marry ambaye ni shahidi wa tatu ameyaeleza hayo wakati akiongozwa na Wakili wa serikali Costantine Kakula, mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu Thomas Simba.

WP Marry amedai kuwa Wema alimueleza maneno hayo wakati walipokuwa njiani kuelekea nyumbani kwake kumkagua.

Amedai kuwa February 4, 2017 aliagizwa kumtoa Wema Mahabusu na kwenda kumfanyia upekuzi nyumbani kwake akiwa na OC CID na Maofisa wengine wa Polisi.

Amedai kuwa wakiwa wanajiandaa kuondoka Central Polisi kuelekea kwa Wema Bunju Basihaya, wakiwa kwenye gari kuelekea huko alimuuliza Wema kuhusu tuhuma zinazomkabili kwamba anahusika na biashara ya Dawa za kulevya au kutumia.

Amedai kuwa Wema alijibu “Sijishughulishi na kuuza ila natumia bangi kama starehe”.

WP Marry amedai kuwa baada ya kumuuliza Wema alimwambia mara yake ya mwisho kuvuta Bangi ilikuwa Jumatatu ambapo swali hilo aliulizwa February 4,2017.

Alieleza kuwa walipofika nyumbani kwa Wema waligonga geti na kufunguliwa na mdada wa kazi ambapo walivyoingia ndani walikuta kuna mdada mwingine wa kazi.

WP Marry amedai kuwa kabla ya kuingia ndani Wema aliomba kumpigia simu dada yake ili awepo wakati wa kufanya ukaguzi ambapo dada yake alifika na kujitambulisha kwa jina la Nuru Sepetu.

WP Marry ameeleza kuwa wakati Wema anampigia simu dada yake alitoka dada mmoja wa kazi kumfuata mjumbe ambapo alikuja naye na kujitambulisha kwa jina la Steven Ndaho.

Amedai baada ya dada yake Wema kufika alitaka kuwapekua kabla ya kuingia ndani ambapo Nuru aliwapekuwa wote kabla ya kuingia ndani.

Amedai baada ya kumaliza upekuzi walirudi Central polis, February 8,2017 saa nne asubuhi alipewa maelekezo na Inspekta Wille kwamba aende na Wema kwa Mkemia Mkuu wa serikali kwa ajili ya kuchukuliwa sampuli ya mkojo.

Baada ya kueleza hayo, Hakimu Simba aliahirisha kesi hiyo hadi March 12 na 13, 2018 kwaajili ya kuendelea na ushahidi.


from MPEKUZI

Comments