WastaraAfunguka Baada ya Rais Magufuli Kumchangia Milioni 15

Msanii wa filamu nchini Wastara Juma amefunguka na kudai hakutegemea kama Rais Magufuli angeweza kulipa kipaumbele tatizo lake alilokuwa kwa sasa huku akimshukuru kwa kuweza kumsaidia suala hilo.

Wastara ameeleza hayo wakati alipokuwa akipokea pesa ya matibabu iliyotolewa na Rais Magufuli na mke wake Mama Janeth jumla ya milioni 15 ili iweze kumsaidia katika matibabu yake kama waliyovyoongea katika simu hapo awali.

"Kubwa niseme tu nashukuru, kwa sababu sikutegemea kama tatizo langu Mhe. Rais angeweza kulipa kipaumbele. Nashukuru pia naomba mpeleke salamu zangu kwa Mhe kwamba natamani siku moja nisimame ili niweze kuwa naye bega kwa bega katika kazi za kujenga nchi yetu ya Tanzania",alisema Wastara.

Pamoja na hayo Wastara ameendelea kwa kusema "natambua kuna watu wengi wana shida, mimi kama mimi natamani nifanye kazi yangu ili niweze kutoa 'percent' yangu niweze kuwasaidia na nimekuwa nikiomba sana muda mwingi jambo hilo".


from MPEKUZI

Comments