Lowasa, Benard Membe Wakutana Uso Kwa Uso

Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa na aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Nje katika Serikali ya Awamu ya Nne, Bernard Membe wamekutaka katika msiba wa mama wa Askofu Mkuu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima.

Membe na Lowassa wamekutana leo Alhamisi Januari 25,2018 nyumbani kwa Askofu Gwajima, Salasala wilayani Kinondoni.

Wawili hao walijitosa katika kura ya maoni ya CCM kuwania kupitishwa na chama hicho tawala kugombea urais katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015.

Katika mchakato huo jina la Lowassa lilikatwa mapema, huku Membe akiwa miongoni mwa wagombea watano waliopitishwa na Kamati Kuu ya CCM. Walishindwa na John Magufuli aliyepeperusha bendera ya CCM katika uchaguzi huo na kuibuka na ushindi.

Ruth Basondole, mama mzazi wa Askofu Gwajima amefariki dunia akiwa na miaka 84.


from MPEKUZI

Comments