Balozi Mulamula Afanya Mkutano Kwa Njia Ya Simu Na Waziri Wa Mambo Ya Nje Wa Sweden


Na Mwandishi wetu, Dar

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula amefanya mkutano kwa njia ya simu na Waziri wa Mambo ya Nje wa Sweden Mhe. Ann Linde katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Viongozi hao pamoja na mambo mengine, wamejadili masuala mbalimbali ya ushirikiano kati ya Tanzania na Sweden ikiwemo vipaumbele vya pande zote mbili kuelekea Mkutano wa Wakuu wa Nchi baina ya nchi za Umoja wa Ulaya na Umoja wa Afrika (European Union – African Union Summit) uliopangwa kufanyika tarehe 17 – 18 Februari 2022.

Katika tukio jingine, Balozi Mulamula amekutana kwa mazungumzo na Balozi wa Somalia nchini Mhe. Zahra Ali Hassan katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam ambapo mazungumzo yao yamelenga kujadili masuala mbalimbali ya ushirikiano kati ya Tanzania na Somalia

 



from MPEKUZI

Comments