Kabendera atakiwa kwenda mwenyewe kwa DPP ili kujua Hatima Yake

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imeuambia upande wa utetezi katika kesi ya uhujumu uchumi inayomkabili Mwandishi wa Habari, Erick Kabendera kuwa waende wenyewe kwa Mkurugenzi wa Mashtaka Nchini (DPP) ili kujua hatma ya barua ya Kabendera ya makubaliano ya kuomba msamaha na kukiri kosa.

Hatua hiyo imefikiwa wakati kesi hiyo ilipoitwa Mahakamani hapo mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Janet Mtega kwa ajili ya kutajwa na kudaiwa kuwa upelelezi bado haujakamilika hivyo upande wa utetezi wakawasilisha hoja zao.

Wakili wa Utetezi, Jebrah Kambole amesema Oktoba 11,2019 waliitaarifu Mahakama juu ya Kabendera kuandika barua ya kuomba msahama na kukiri kosa kwenda kwa DPP lakini mpaka leo ni miezi miwili hawajapata mrejesho wowote kutoka kwa DPP na Mtuhumiwa bado yuko gerezani na ni mgonjwa.

Kufuatia hoja hizo, Hakimu Mtega ameutaka upande wa utetezi waende wenyewe kufuatilia jalada la kesi kwa DPP ili wajue kinachoendelea na ameiahirisha kesi hiyo hadi itakapotajwa tena Desemba 18, mwaka huu.


from MPEKUZI

Comments