Mhadhiri wa Chuo cha Usafirishaji (NIT) Samson Mahimbo Afikishwa Mahakamani Kwa Kuomba Rushwa ya Ngonoi Kwa Mwanafunzi Ili Amsaidie Kufaulu

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu leo Agosti 14, imemuachia kwa dhamana mhadhiri wa Chuo cha Usafirishaji (NIT) Samson Mahimbo anayekabiliwa na mashtaka ya kuomba rushwa ya ngono kutoka kwa mwanafunzi wake.

Mshtakiwa hayo amesomewa mashtaka mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi na Wakili kutoka TAKUKURU ambapo inaelezwa kuwa mshtakiwa alitenda kosa hilo Januari 12, 2017.

Imeelezwa kuwa mshatakiwa alitenda kosa hilo akiwa katika nyumba ya kulala wageni ya Com David iliyopo katika maeneo ya Mlalakuwa, Mwenge, kwa kumlazimisha mwanafunzi wake kutoa rushwa ya ngono kwa madai ya kwamba angemsaidia ufaulu katika masomo yake.

Mara baada ya kusomewa mashtaka hayo, mshtakiwa alikana kutotenda kosa hilo na upelelezi wa kesi hiyo haujakamilika na kuahirishwa hadi Septemba 17, 2019. Mshtakiwa yupo nje kwa dhamana.


from MPEKUZI

Comments