RPC Shinyanga athibitisha Tukio la kushambuliwa na kudhalilishwa kwa Mshiriki wa Miss Shinyanga 2019.

SALVATORY NTANDU
Jeshi la mkoani Shinyanga limethibitisha kuwepo kwa tukio la kushambuliwa kwa mwanamitindo, Nicole Emanuel (19) mshiriki wa Miss shinyanga 2019 kushambuliwa na waandaaji wa shindano hilo na kumsababishia majeraha katika sehemu mbalimbali za mwili wake.

Kamanda wa Polisi mkoa humo, (ACP) Richard Abwao amesema kuwa tukio hilo limetokea julai 11 mwaka huu katika hoteli ya Nedman iliyopo mjini Shinyanga.

Amewataja waliohusika kumshambulia na kumshalilisha  Nicole ni pamoja na mkurugenzi wa  Makumbusho  Entertainment, Richard Luhende ambaye pia ni mwenyekiti wa Chama Kikuu cha Ushirika (SHIRECU) mkoa wa Shinyanga na Meneja Mkuu wa Makumbusho Entertainment, George Foda.

Amesema watuhumiwa wanadaiwa kumshambulia kwa kupigwa ngumi, mateke, kuburuzwa na kisha kuchaniwa nguo zake jambo ambalo kumsababishia majeraha  maumivu makali baada ya Nicole kwenda kuwadai fedha za  nauli na gharama alizotumia katika shindano la miss Shinyanga.


from MPEKUZI

Comments