Wagonjwa 1,901 wa Dengue wabainika

Jumla  ya wagonjwa 1,901 wamebainika kuwa na virusi vya  homa ya Dengue, tangu kuibuka kwa ugonjwa huo nchini, Januari mwaka huu.

Kati ya wagonjwa hao, 1,809 ni wakazi wa jiji la Dar es Salaam, 89 kutoka Tanga mmoja kutoka Singida, mmoja Kilimanjaro na mmoja kutoka mkoani Pwani.

Mganga Mkuu wa Serikali wa Wizara ya  Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Prof. Mohammed Kambi, ameyasema hayo jana jijini Dar es Salaam wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu hali ya ugonjwa huo nchini

Amesema kwa mujibu wa taarifa ya siku tisa hadi jana, kuna ongezeko la wagonjwa 674 sawa wastani wa wagonjwa 75 kwa kila siku, ikiwa ni tofauti ya wastani wa wagonjwa 32 waliopatikana Aprili mwaka huu.

Amesema wagonjwa wawili waliopatikana katika mikoa ya Kilimanjaro na Pwani wametoka jijini Dar es Salaam.

"Ongezeko hili linatokana na kuongezeka kwa uelewa kuhusu ugonjwa huu kwa wananchi walio wengi wenye dalili na hivyo wanajitokeza kupata huduma za uchunguzi ambazo zimeendelea kupanuka kwenye vituo vyetu katika mkoa wa Dar es Salaam na Tanga," amesema Prof. Kambi.

Ametaja Idadi ya vituo vinavyopima ugonjwa huo imeongezeka hadi kufikia 19 tofauti na vituo saba vilivyokuwapo awali.


from MPEKUZI

Comments