Rais Magufuli Awataka Viongozi Anaowateua Washirikiane

Rais wa Tanzania John Magufuli amewataka viongozi wa kuteuliwa kuanzia ngazi ya ukuu wa mkoa mpaka ngazi za chini kujenga ushirikiano na uhusiano mzuri baina yao ili kurahisisha utekelezaji wa majukumu yao, vinginevyo hatasita kuchukua hatua.

Wito huo umetolewa kwa wakuu wa mikoa, makatibu tawala wa mikoa, wakuu wa wilaya, makatibu tawala wa wilaya na wakurugenzi wa halmashauri za wilaya, miji, manispaa na majiji.

Rais Magufuli ametoa maelekezo hayo jana Mei 16, 2019 katika kikao kazi kati yake na viongozi hao kilichofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam.

Amewaonya baadhi ya viongozi hao ambao wamekuwa na migogoro baina yao na hivyo kuathiri utendaji kazi na amesema endapo vitendo hivyo vitaendelea hatasita kuchukua hatua ikiwa ni pamoja kuwaondoa katika nyadhifa zao.



from MPEKUZI

Comments