Mnyika Ataka Baraza la Mawaziri Livunjwe

Mbunge wa Kibamba John Mnyika (Chadema) ,amemwomba Rais Dk.John Magufuli alivunje Baraza la Mawaziri kwa kumshauri vibaya katika suala la Korosho.

Kauli hiyo ameitoa leo bungeni Mei 20 wakati akichangia mjadala wa Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, kwa mwaka wa fedha 2018-2019.

Mnyika amesema Baraza la Mawaziri linatakiwa kuwajibishwa kwa kumshauri vibaya Rais Dk.John Magufuli katika suala la Korosho kwani kwa sasa Korosho inaoza kutokana na kukosekana kwa wanunuzi.


from MPEKUZI

Comments