Mamia ya wanachama CUF Kutoka Kata 27 na Matawi 96 Tanga wahamia ACT-Wazalendo Kuungana na Maalim Seif

Wanachama wa Chama cha Wananchi (CUF) jijini Tanga, kutoka kata 27 na matawi 96, wamemfuata aliyekuwa Katibu Mkuu wa chama hicho, Maalim Seif, ACT- Wazalendo na kukabidhiwa kadi za uanachama.

Wakati wanachama hao wakifanya uamuzi huo, leo Jumanne Machi 19, jijini Dar es Salaam, Maalim Seif amekabidhiwa rasmi kadi namba moja ya ACT-Wazalendo iliyolipiwa ada ya miaka 10.

Wanachama hao pia, wamechoma kadi zao za zamani na bendera za CUF, kuashiria kwamba wamejivua uanachama wa chama hicho na sasa wao ni rasmi wanachama wa ACT-Wazalendo.

Wamesema wameamua kumuunga mkono maalimu Seif kujiunga ACT Wazalendo kwani ndio chama makini kinachoweza kuwafikisha kwenye azma yao ya kuiondoa CCM madarakani.


from MPEKUZI

Comments