Godbless Lema Kesho Atazungumza na Waandishi wa Habari Kuhusu Sakata La Mo Dewji Kutekwa

Mbunge wa Arusha Mjini (Chadema), Godbless Lema amesema amekamilisha uchunguzi wa sakata la kutekwa kwa mfanyabiashara maarufu nchini, Mohammed Dewji ‘Mo’ na kesho atazungumza.

Lema ambaye pia ni Waziri Kivuli wa Mambo ya Ndani, amesema mkutano huo na waandishi utafanyika makao makuu ya Chadema mtaa wa Ufipa, Kinondoni jijini Dar es Salaam.

Familia ya mfanyabiashara maarufu nchini, Mohammed Dewji ‘Mo’ leo imezungumza na waandishi wa habari kuhusu kutekwa kwa bilionea huyo na kutangaza dau la Sh1 bilioni kwa mtu yeyote atakayewezesha kupatikana kwake.



from MPEKUZI

Comments