Chadema wakanusha kuwepo mgogoro ndani ya chama

Chadema kimekanusha taarifa zinazosambaa kwenye mitandao ya kijamii kuwa mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe na Katibu Mkuu Dk Vincent Mashinji wametofautiana kwenye kikao cha Kamati Kuu.

==>>Hapo chini ni taarifa ya CHADEMA
Ndugu waandishi, Zipo taarifa potofu zinasambaa kwenye mitandao ya kijamii kuwa Mwenyekiti wa Chama Mhe.Freeman Aikaeli Mbowe na Katibu Mkuu Dr.Vincent Mashinji wametofautiana kwenye kikao cha Kamati Kuu kilichofanyika nyumbani kwa Mwenyekiti mwishoni mwa juma hili.

Napenda kutoa ufafanuzi kama ifuatavyo;

1. Hakuna kikao chochote cha Kamati Kuu ambacho kimefanyika mwishoni mwa wiki hii, sio tu nyumbani kwa Mwenyekiti Mbowe bali Popote pale.

2. Hakuna Popote ambako viongozi hao waandamizi wametofautiana kuhusu yanayoendelea kwenye mitandao ya kijamii.

3. Haijawahi kutokea wakati wowote Vikao vya kamati kuu vikafanyika nyumbani kwa Mwenyekiti wa Taifa

4. Tunaomba watanzania na Wanachama wetu wapuuze taarifa hiyo potofu inayosambazwa kwenye mitandao.

John Mrema
Mkurugenzi wa Itifaki, Mawasiliano na Mambo ya Nje.
15 Oktoba, 2018
 


from MPEKUZI

Comments