Mwili wa Mtangazaji Dr Misanya Bingi Waagwa na Kusafirishwa Kuelekea Dodoma Kwa Mazishi

Mwili  wa aliyekuwa mtangazaji mahiri nchini na Mhadhiri wa Shule ya Habari na Mawasiliano ya Umma (SJMC) iliyo chini ya Chuo Kikuu Dar es Salaam (UDSM), Dkt Misanya Bingi (47) umeagwa leo katika Kanisa Katoliki la Makongo Juu liliopo Dar es Salaam na kusafirishwa kuelekea Miuji jijini Dodoma kwa ajili ya mazishi siku ya kesho.

Dkt Misanya Bingi alifariki dunia siku Jumapili katika Hospitali ya Taifa Muhimbili na wakati wa uhai wake alifanya kazi kwenye kituo cha Radio One ambapo alitangaza vipindi mbalimbali.



from MPEKUZI

Comments