Breaking News: Mbunge Mwingine CUF Ajivua Uanachama na Kuhamia CCM

Mbunge mwingine toka Chama cha Wananchi CUF jimbo la Liwale, Zuberi Kuchauka kwa hiari yake mwenyewe  ameamua kujivua uanachama wa chama hicho na kujiunga na Chama cha Mapinduzi CCM

Ametangaza uamuzi huo leo August 12, 2018  katika mkutano wa waandishi wa habari uliofanyika katika ofisi ndogo za CCM Lumumba jijini Dar es Salaam, akiwa sambamba na Katibu Mkuu wa chama hicho tawala, Dk Bashiru Ally.

Kuchauka amesema moja ya sababu iliyomuondoa CUF ni utendaji kazi wa Rais John Magufuli pamoja na mgogoro unaokitafuta CUF.


from MPEKUZI

Comments