Ay na mkewe Wapata Mtoto Wa Kiume

Ikiwa imepita miezi sita tangu mwanamuziki, Ambwene Yessayah (AY) na Remy wafunge ndoa usiku wa kuamkia Jumatatu Agost 13,2018 leo wamebarikiwa kupata mtoto wa kiume waliyempa jina la Aviel lenye maana kwamba ‘God is my father’,.

Jumatatu hii rapa huyo ameutaarifu umma kwamba mke wake huyo amepata mtoto wa kiume aitwaye Aviel.

“Mungu ni mwema na namshukuru sana kwa kutubariki mimi na My Beautiful Wife #Remy tarehe 12.08.2018 Medical City Healthcare Dallas -Texas tumepata mtoto wa kiume AVIEL maana yake GOD IS MY FATHER…. 3.9Kgs & 27 inches…Welcome to the World AVIEL YESSAYAH πŸ™πŸΏπŸ™πŸΏπŸ™πŸΏπŸ™πŸΏπŸ™πŸΏ,” aliandika rapa huyo kupitia instagram yake.

AY na Remy ambae ni raia wa Rwanda walifunga ndoa Februari 24,mwaka huu jijini Dar es Salaam ambapo kulihudhuriwa na mastaa kibao.


from MPEKUZI

Comments