Afisa Habari wa Yanga Dismas Ten akanusha kujihuzulu yanga

Na Magdalena Kashindye
Afisa Habari wa Yanga Dismas Ten amekanusha taarifa zinazosambaa kuwa amejiuzulu nafasi yake.

Ten ambaye alikuwa nje ya ofisi kwa wiki kadhaa kutokana na kuugua maradhi yaliyosababisha akalazwa, amesema yeye bado ni mwajiriwa wa Yanga.

"Bado tupo mapambano yanaendelea "-Ten ameandika kwenye akaunti yake ya instagram

Baadhi ya vyombo vya habari vimeripoti kuwa Ten amejiuzulu nafasi yake baada ya kuenea taarifa za kujiuzulu kwa Katibu Mkuu, Charles Mkwassa.

Taarifa hizo zimebainisha kuwa Ten amejiondoa Yanga sababu kuu ikielezwa kukosa ushirikiano kutoka kwa baadhi ya viongozi wa mabingwa hao wa Kihistoria Tanzania Bara.


from MPEKUZI

Comments