StarTimes yazindua Wasafi TV kwenye king’amuzi chake.

Wapenzi wa burudani kote nchini ni wakati wao kufurahia baada ya Kampuni ya Star Media (T) Ltd kupitia chapa yake ya StarTimes kutangaza rasmi kwamba chaneli ya Wasafi TV imeanza kuonekana kupitia king’amuzi chake. 

Uzinduzi wa chaneli ya Wasafi TV kwenye king’amuzi cha StarTimes umefanyika Jumatatu tar 18 katika Hotel ya Slipway, Masaki jijini Dar es Salaam.

Sasa chaneli hii mpya ya Burudani itaweza kutazamwa na watu wengi zaidi Tanzania kwa sababu StarTimes ndicho king’amuzi chenye watumiaji wengi zaidi hapa nchini kuliko kingine chochote.

“Kuanzia sasa Wasafi TV itapatikana katika ving’amuzi vyetu vya Antenna, kwa hiyo watumiaji wa Antenna wanaweza kutazama chaneli hii mpya ikiwa na vipindi vipya ambavyo vitatangazwa baadaye. 

"Pia wateja wanaweza kulipia kifurushi chochote cha Antenna kuipata Wasafi TV, unaweza kulipia NYOTA kwa 7000 tu mwezi mzima, MAMBO Tsh 13,000 tu kwa mwezi na UHURU kwa 24,000 tu. 

"Wasafi TV kwa sasa inapatikana kwenye Antenna pekee, na muda wowote kuanzia sasa itakuwa tayari kwa watumiaji wa ving’amuzi vya dish pia”, Ndg David Malisa, Meneja Masoko wa StarTimes.


from MPEKUZI

Comments