Macho Yote ya Waafrika Leo Nchini Urusi ni Kwa NIGERIA Itayokabiliana na Croatia

Michuano ya Kombe la Dunia inaendelea tena leo Jumamosi kwa viwanja vinne kuwaka moto nchini Urusi.Katika mechi za jana, timu zote kutoka Afrika zilifanya vibaya kwa kupoteza michezo yake ya kwanza kwa bao 1-0.

Misiri iliyojitupa dimbani bila nyota wake Mo Salah ilifungwa mnamo dakika za mwisho na Uruguay huku Morocco nayo ikiambulia maumivu kwa bao moja pekee la kujifunga dhidi ya Irani.

Timu pekee kutoka Afrika leo, Nigeria, inapewa nafasi ya kutufuta machozi waafrika wote endapo itafanikiwa kuibuka na ushindi  dhidi ya Croatia kuanzia saa NNE  usiku.

Kwa upande wa Croatia, hawana majeruhi na wanategemea kutaja mastaa wote wakiwemo Luca modric,Ivan Rakitic,Vedran Corluka na Mario Mandzukic.

Mshambuliaji wa Croatia Nikola Kalinic amesema, Kitu muhimu sasa ni pointi zote tatu.

Kwa Upande wa Nigeria, Mlinzi wa Nigeria, Leon Balogun, anaweza kukosa mechi baada ya kukosa mazoezi yaliyofanyika Alhamis, na Kenneth Omeruo anasubiri mchezaji Wilfred Ndidi ili aweze kuchukua nafasi yake, pamoja na kwamba alikuwa ana majeraha,Odion Ighalo anaweza kuiongoza safu ya ushambuliaji, akishirikiana na Khelechi Ihenacho.

Kocha wa Nigeria Gemot Rohr anasema, "Timu tunayo kwa muda mrefu, tulikuwa nayo pia kwenye mechi za kufuzu, Nina uhakika tutawafanya Wanaigeria wafurahi."


from MPEKUZI

Comments