PICHA: Wasafi Tv Wazindua Kipindi Cha Mwezi Mtukufu Wa Ramadhani

Kituo cha televisheni cha Wasafi Tv kinachomilikiwa na staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz, siku ya jana kimetangaza ujio wa kipindi cha mwezi mtukufu wa Ramadhani.

Siku ya jana Wasafi Tv walifanya uzinduzi wa kipindi hiko kitakachoitwa Nyumba ya Imani ambacho kitakuwa maalumu kabisa kwa waislamu wote katika mwezi huu mtukufu wa Ramadhani kitakachorushwa Wasafi Tv.

Hafla hiyo ilifanyika katika makao makuu ya Wasafi Tv Mbezi beach na kuhudhuriwa na mastaa mbali mbali walioalikwa kwa ajili ya kupata futari.

Hizi ni baadhi ya picha za hafla hiyo:


from MPEKUZI

Comments