Msigwa Amtaka Dk. Kigwangala Kutoa Ushahidi Wa Ufisadi Wake

Mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa amemtaka Waziri wa Maliasili na Utalii, atoe ushahidi bungeni juu ya ufisadi wake pamoja na aliyekuwa waziri wa wizara hiyo Lazaro Nyalandu.

Msigwa amesema hayo bungeni leo Mei 21, alipokuwa akichangia bajeti ya wizara hiyo, kwa mwaka wa fedha 2018/19 iliyowasilishwa na Dk. Kigwangala.

Kwa mujibu wa Msigwa, tuhuma dhidi yake na Nyalandu zilizotolewa na Dk. Kigwangala miezi michache iliyopita haziwezi kufumbiwa macho kwa sababu zilichafua majina yao katika jamii.

“Namuomba Dk. Kigwangala alieleze bunge amenufaika kiasi gani kupitia kwa mfanyabiashara OBC aliyeko Loliondo kwa kuwa hivi karibuni alionekana akipokea magari kwa ajili ya kukabiliana na majangili,” amesema Msigwa


from MPEKUZI

Comments