Wachunguzi wa sumu Hatimaye Wameruhusiwa Kuingia Syria

Wachunguzi wa kimataifa leo Aprili 18 wameingia katika mji wa Syria uliokumbwa na kile kinachodaiwa kuwa ni shambulizi la sumu.

Hata hivyo, wachunguzi hao wanaingia nchini humo ikiwa ni  siku kadhaa za kucheleweshwa na onyo kutoka kwa mataifa ya magharibi kuwa ushahidi muhimu huenda umeshaondolewa.

Shirika la habari la Syria - Sana limesema wataalamu  hao kutoka Shirika la Kimataifa la Kudhibiti Silaha za Sumu -OPCW wameingia mjini Douma.

Shambulizi hilo linalodaiwa kuwa la gesi mnamo Aprili  7 mjini Douma, karibu na Damascus, liliripotiwa kuua zaidi ya watu 40.

Mataifa ya magharibi yalimtuhumu Rais wa Syria Bashar al-Assad kwa tukio hilo.

 Watalaamu hao waliwasili Syria siku ya mashambulizi ya nchi za magharibi lakini wakazuiwa kuingia Douma.


from MPEKUZI

Comments