Usambazaji wa gesi Majumbani kuanza kesho jijini Dar


Usambazaji wa gesi majumbani katika jiji la Dar es Salaam unaanza kesho Jumanne, Aprili 24 huku bei ya gesi ikipungua kwa asilimia 40 ya bei ya sasa kwenye mitungi.

Waziri wa Nishati, Dk Medadi Kalemani ametoa kauli hiyo muda mfupi  wakati akijibu hoja za Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG)  katika utaratibu wa mawaziri waliojiwekea.

Dk Kalemani amesema gharama za kuunganisha gesi kwa wateja watakaopitiwa na bomba hilo itakuwa Sh 200,000 hadi 1 milioni kutegemeana na umbali kutoka lilipo bomba kuu.

Ametaja baadhi ya maeneo yatakayoanza kunufaika kuanzia kesho ni Ubungo, Mwenge, Kijitonyama, Gongolamboto, Shekilango na Mikocheni na kazi hiyo itadumu kwa miezi miwili.


from MPEKUZI

Comments