Rais Magufuli Ateua Mwenyekiti Bodi ya Wakurugenzi Benki ya Posta

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amemteua Dkt. Edmund Bernard Mndolwa kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya Posta Tanzania (TPB).

Uteuzi wa Dkt. Mndolwa umeanza leo tarehe 23 Aprili, 2018.

Dkt. Mndolwa anachukua nafasi ya Prof. Lettice Rutashobya ambaye amemaliza muda wake.



from MPEKUZI

Comments