Polisi waua majambazi wanne Pwani

Majambazi wanne wameuawa  na polisi asubuhi ya leo Ijumaa Aprili 20, wakati wakijaribu kupora Kisarawe mkoani Pwani.

Kabla ya kuuawa yalitokea majibizano ya risasi kati yao na askari Polisi.

Imedaiwa majambazi hao wametokea jijini Dar es Salaam na walikuwa wanatumia gari lenye namba za kibalozi hatua iliyosababisha askari wa usalama barabarani kutowahisi chochote kwani gari hizo sio rahisi kusimamishwa ovyo.

Mkuu wa Mkoa wa Pwani, ambaye pia ni Mwenyekiti Kamati ya Ulinzi na Usalama mkoani Pwani, Evarist Ndikilo amethibitisha tukio hilo.


from MPEKUZI

Comments