Mwili wa Masogange kuagwa Leaders, kuzikwa Mbeya

Video queen maarufu Bongo Agnes Gerald maarufu Kama Masogange anatarajiwa kuzikwa nyumbani kwao Wilayani Mbozi, mkoani  Mbeya ambako ndiko wazazi wake waliko.

Dada wa Agnes anayejulikana kama Emma Gerald, amesema mwili wa Agnes utaagwa jijini Dar es salaam kwenye viwanja vya Leaders Club Kinondoni siku ya kesho Jumapili kuanzia saa 3:00 asubuhi.

Ambapo misa itafanyika viwanjani hapo kisha kuanza safari rasmi kuelekea Mbalizi mkoani Mbeya kwa ajili ya kuupumzisha mwili wa marehemu Agnes Gerald mahali pema peponi.

“Tutaaga kesho asubuhi saa 3 pale Leaders, na kisha tutasafirisha kuelekea Mbeya kwa mazishi”, amesema Emma Gerald.

Aidha imeelezwa kuwa kutakuwa na mabasi mawili yatakayobeba wasindikizaji wa mwili huo mpaka mkoani Mbeya.

Agnes Masogange amefariki jana Aprili 20, kwenye hospitali ya Mama Ngoma baada ya kulazwa kwa muda wa siku nne mpaka kifo kilipomkuta kwa tatizo la pumu.


from MPEKUZI

Comments