Diva Ammwagia Mvua Ya Matusi Ya Nguoni Michael Lukindo

Msanii na mtangazaji wa kipindi cha Ala za roho cha Clouds Fm Loveness Malinzi ‘Diva The bawse’ amemtolea povu zito msanii mwenzake wa Bongo fleva Michael Lukindo ‘ML’ baada ya kudai ni wapenzi.

Siku chache zilizopita Michael Lukindo alifanya mahojiano na XXL ya Clouds Fm na alikuwa anatambulisha ngoma yake mpya lakini Kwenye mahojiano hayo alifunguka kuwa yupo Kwenye Mahusiano na Diva.

Baada ya kusikia taarifa hizo Diva alitumia ukurasa wake wa Instagram na kumwaga povu zito na kukataa kata kata kama yupo Kwenye Mahusiano ya kimapenzi na Michael Lukindo.

Baada ya Tetesi hizo kusambaa Soudy Brown alimsaka Michael ambaye alikiri kuwa alikuwepo Kwenye Mahusiano na Diva lakini walifanya siri na mpaka sasa Diva hayupo tayari kuzungumzia hayo mahusiano.

Baada ya kusikia maneno hayo Diva ambaye kwa muda huo alikuwa studio alimtolea matusi mazito Michael Lukindo:

"Wewe mata** unikome shika adabu yako umeshawahi kuwa na Mahusiano na mimi lini na wapi?na nilikwambia kabisa kwamba nimekushtaki I have defamation letter for you utajifunza kufunga huo mdomo wako sitaki mambo ya kise*** k*** la mama ako umeenda umemzungumzia Jokate on the same same thing haukutosheka ukamuandika Miriam Odemba kuwa una Mahusiano naye sasahivi unataka kwangu mimi kunitafutia kiki sasa mimi ntakukomesha nimeshakushtaki”.


from MPEKUZI

Comments