Wastara Amchana Mange Kimambi....."Ana Cheti Cha Mirembe"

Msanii wa maigiizo nchini Wastara Juma amefunguka na kuongelea yaliyokuwa yanajiri alipokuwa hospitali na kusema kuwa kipindi yupo katika matibabu yake nchini india , mwanaharakati Mange kimambi aliwapigia simu madaktari na kuwadanganya kuwa ni dada wa Wastara na kutaka kujua  details zake.

Wastara alisema hayo alipokuwa akifanya mahojiano katika kipindi cha kikaangooni live  kinachorushwa na EATV,  Ambae alizusha uongo mwingi kuhusu matibabu ya msanii huyo baada ya kuonekana kwa cannula ambae ilisemekana kuwa imegeuzwa kwa mujibu wa Mange ingawa Wastara mwenyewe alikataa swala hilo.

"Mange kimambi aliwahoji madaktari nikiwa india,mimi nikashaanga kuona madaktari wanakuja wananiuliza mimi ni nani Tanzania, nikawajibu mimi ni msanii ....wakaniuliza  kama ninamfahamu huyu mtu anaitwa Mange Kimambi anasema kuwa ni dada   yangu, na pa ni mwamndishi wa habari anakuulizia, nikawajibu sina dada mwenye cheti cha milembe."

Wastara anasema kuwa kama mange kimambi angekuwa na akili basi alitakiwa kuangalia ile cannula vizuri kabla ya kuanza kuweka maneno katika mitandao kuhusu kudanganya


from MPEKUZI

Comments