Viongozi Watatu Mtandao wa wanafunzi Tanzania (TSNP) Waitwa Polisi

Viongozi watatu wa nafasi za juu katika Mtandao wa wanafunzi Tanzania (TSNP) wameitikia wito wa kufika kwa mpelelezi wa makosa ya Jinai (DCI) Jijini Dar es Salaam leo asubuhi kwa lengo la kuhojiwa kutokana na tukio la Abdu Nondo.

Hayo yamebainishwa na taarifa iliyotolewa na Afisa Habari- TSNP, Hellen Sisya baada ya kupita siku moja tokea Jeshi la Polisi kupitia Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa kuwataka viongozi hao kufika katika ofisi za DCI.

"Tumepokea taarifa ya Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam inatofautiana kabisa na ile ya Iringa juu ya kuonekana kwake. Hata hivyo, kabla ya taarifa ya uchunguzi kulitanguliwa na matamko ya viongozi wa juu waliodai kuwa Abdul Nondo alijiteka mwenyewe jambo ambalo kwa vyevyote lingeathiri uchunguzi wa jeshi la polisi", amesema Hellen.

Pamoja na hayo, Hellen ameendelea kwa kusema "pamoja na mapungufu yote tunaamini Nondo atatendewa haki atakapofikishwa mahakamani".

Kwa taarifa kamili soma hapa chini.


from MPEKUZI

Comments