TANGA RAHA- Sehemu ya Thelathini na Saba ( 37 )

AGE………………18+
WRITER…………EDDAZARIA G.MSULWA
ILIPOISHIA

Nilizungumza kwa sauti ya kujiminya kwani mfuniko ulituzidi nguvu,Mzee ngoda akajiingiza katikati yetu na kutusaidia kuufungua mfuniko na kwa pamoja tukafanikiwa kuufungua.Gafla tukastukia kumuona Mzee Ngoda akirushuwa juu kama kifaranga kilicho nyakukiliwa na Mwewe mwenye njaa kali na kitendo cha kutua chini hakuwa na kichwa na damu nyingi zikawa zinaruka kila sehemu na kumfanya Rahma kupiga ukulele mkali

ENDELEA
Nikabaki nikiutazama mwili wa mzee Ngoda jinsi unavyo rusha rusha miguu,Sauti kali nikaisikia kwenye masikio yangu ikiniambia
“Mmoja wenu ni lazima afee”
Nikayakumbuka yalikuwa ni maneno ya bibi,kwa haraka nikamuwahi kumziba mdomo Rahma.
“Shiii nyamaza”
Nikaendelea kumziba mdomo Rahma kwa nguvu kwa kutumia kiganja cha mkono.Tukayashuhudia majini yakitoka na kulizunguka eneo tulilopo sisi huku wakiwa wanaelea elea angani.Nikakitoa kifimbo mfukoni na kuwanyooshea majini yaliyojaribu kwenda mbali,

“RUDINI HAPA”
Nilizungumza kwa sauti ya ukali na majini hayo yakatii,hadi na mimi nikaanza kushangaa.Rahma akanikumbatia kwa nyuma,mwili mzima ukiwa unamtetemeka mithili kama amepigwa shoti ya umeme.Eneoa la anga zima katika eneo tulilopo limefunikwa na majini haya ambayo ni mengi sana na yana sura za kila aina
“Tunakushukuru sana kwa kututoa”
Niliisikia sauti kwenye masikio yangu ambayo ni tofauti sana usikiaji wake kama tulivyo sisi wanadamu,Kwani sauti niliisikia ndani ya masikio yangu na si kama ile inayo ingia kwenye masikia yangu.Nikawatazama kwa umakini na kuwashuhudia wakiwa akatika makindi tofauti tofauti,Wazee sana,wazee kiasi,vijna na watoto
“Munataka nini?”
“Tulikuwa tunauhitaji uhuru,tumeupata kutoka kwako asante sana,tupo tayari kukusikiliza wewe kwa kila kitu”
Hata jini ambaye ananijibu simjui ni yupi kati ya kundi kubwa ambalo limetuzingira mimi na Rahma

“Kwa leo tunakuomba tutoke tukatafute japo kitu cha kula,kisha saa kumi na mbili tutakuwa tumerudi”
“Eddy ukiwaruhusu hawa huko kwengine mambo yatakuwa si mazuri”
Rahma aliniambia
“Kumbe hata wewe unawasikia?”
“Ndio”
“Sasa munaniahidi nini nikiwaruhusu kwenda kuchukua chakula?”
“Amani itakuwa juu yetu”
“Hamuto wadhuru wanadamu wengine kama huyu?”
“Hatuwezi fanya hivyo,tunakuahidi”
Nafsi moja inaniambia niwaruhusu na nyingine inaniambia nisiwaruhusu.Nikamtazama Rahma akatingisha kichwa nisiwaruhusu.
“Acha wakatafute kitu cha kula,unadhani hapa wakikaa watakula nini?”
“Haya kama umeoamua hivyo”
“Haya nendeni ila saa kumi na mbili jioni nawahitaji hapa”
“Turuhusu tuanze na mwili huu.”
“Khaaa”

 


from MPEKUZI

Comments