TANGA RAHA- Sehemu ya Thelathini ( 30 )

AGE………………18+
WRITER…………EDDAZARIA G.MSULWA
ILIPOISHIA

    Maneno yangu niliyazungumza kwa uchungu huku nikiwa ninatokwa na machozi na nikapiga hatua mbili mbela na kustukia mlio wa bastola na kujikuta nikiwa nimeanguka chini huku taratibu nikimshuhudia Rahma akianguka huku akiwa amejishika tumboni akitoa kilio cha maumivu makali hii ni baada ya Rahma kunivuta mimi pembeni na yeye kupigwa na risasi ambayo baba yake aliifyatua kwa lengo la kunipiga mimi ili kuniua

ENDELEA
Sote tukabaki tukimshangaa Rahma anaye anguka chini taratibu,nikajikongoja taratibu huku nikitambaa taratibu nikijaribu kuunyoosha mkono wangu mmoja ili kumshika Rahma na kabla sijamfikia nikastukia miguu yangu ikishikwa na lile jitu jeusi na kuanza kuniburuza kwenye majani na kuwaacha wazazi wa Rahma wakimbeba mtoto wao na kumuingiza kwenye gari huku damu zikimvuja.Jamaa likazidi kunivuta na kunitokomeza msituni na mbaya zaidi kila anavyo niburuza ndivyo jinsi ninavyozidi kupata michubuko huku miba mikali aina ya mbigili ikiingia mwilini mwangu na kuzidi kuniogezea maumivu makali.Jamaa akaanza kunipiga mateke ya tumboni kiasi kwamba nikahisi ndio mwisho wa maisha yangu

Jamaa akatoa kamba aina ya manila na kunifunga kwenye miguu na mikononi kisha akarudi sehemu walipo wazazi wa Rahma na nikaanza kujaribu kujifungua kamba kwa kutumia meno ila kutokana na kwa jinsi alivyo ikaza nikajikuta nikishindwa kujifungua,Nikamuona jamaa akirudi huku mkononi mwake akiwa ameshika chepe na sururu na nikazidi kuogoa na sijujua analengo gani.Jamaa akaviweka vitu vyake pembeni na kuanza kuchangu majani kwa kutumi mguu wake wa kulia ulio valia buti kubwa.Nikapata jibu la jamaa kuja na vifaa vyake baada ya kuanza kuchimba shimo kwa kutumia sururu huku chepe akilitumia kwa kutolea ichanga.

“Ohhh Mungu wangu ninakuomba uniongoeze wewe ndio kila kitu kwagu na kuomba huyu jamaa abadilieshe mawazo asinizike nikiwa hai mimi”
Nilizungumza kwa uchungu huku machozi yakinimwagika nikajaribu kujifungua kamba ila nikashindwa na kujikuta nikiwa nimetulia huku nikilia na kujutia ni kwanini nimekuwa na mahusianao na Rahma.
“Kaka....Kaka....Kaka”
Niliita na jamaa akaniangalia kwa macho makali ambayo kwa muonekano wake anavuta bangi kiasi kwamba macho yake ni mekundu kiasi,
“Ndugu yang...u tambua kuwa m...imi na wewe ni wa..tanzania...Pia sisi ni wanaume haya mambo leo hii yana..nipa..ta mimi ila kesho yanaw...eza ya katokea kwako kwa m....fumo mwengine nakuoma ndugu yangu nifu..ngue niweze kuondoka”
Jamaa akanitazama kwa jicho kali kisha akashika chepe lake na kuendelea kutoa mchanga kwani tayari ufefu wa shimo analo lichimba umefikia usawa wa kiono chake,Jamaa akavua shati lake kabisa na kubaki kifua wazi na kuendelea kuchimba shimo huku akifanya haraka.



from MPEKUZI

Comments