AISIIIII……….U KILL ME ( Sehemu ya 57 na 58 )

MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA
ILIPOISHIA 

Nikaona gari tatu za ikulu ambazo anatembelea raisi zikiwa zimesimamishwa kwenye maegesho huku walinzi walio valia suti nyeusi wakiranda randa kika eneo.  Nikamuona Babyanka akitoka kwenye mlango wa jumba hili la kifahari, akamuita mmoja wa walinzi na kuzungumza naye kisha akageuza kuchwa chake na kutazama sehemu nilipo na macho yetu yakakutana jambo lililo mfanya Babyanka kuchomoa bastola yake na kuanza kufyatua risasi kadhaa kueleka sehemu nilipo.

ENDELEA
Nikajiachia na kwenye ukuta na kutua chini kwa umakini wa hali ya juu, nikaanza kukimbia kwa kasi kuelea kwenye mti nilipo iacha pikipikia. Nikafanikiwa kufika, nikashuhudia gari mbili za ikulu zikitoka nje ya geti hilo kwa kasi sana jambo lililo nifanya niiwashe pikipiki yangu kwa haraka na kuondoka eneo hili kwa kasi huku, huku gari hizo kutoka ikulu zikinifwata kwa nyuma. Sikuwa na namna ya kufanya zaidi ya kukatiza vichochoro na nikafanikiwa kupotezana na gari  hizo kwa umbali mkubwa.

Sikuwa na namna ya kuendelea kuwepo katika eneo hili la Tegeta, moja kwa moja nikarudi hadi Sinza kwa mama Marima, pikipiki nikaisimamisha pikipiki sehemu nilipokuwa nimemsimamisha dereva bodaboda. Nikaanza kutembea kwa miguu huku nikiwa makini, gari langu nikalikuta nje likiwa kama nilivyo liacha hapakuwa na tofauti yoyote.
Nikainga ndani na kumgongea mama Marim dirishani kwake. Nikamsikia akifungua mlango wa chumbani kwake, kisha akaufungua mlango wa mbele katika hii nyumba. Tukaingia chumba kwa mama Marim na akafunga milango yote.
“Vipi?”
Mama Marim aliniuliza huku akinitazama usoni.
“Wale wasichana wanafanya kazi chini ya raisi, na muda wowote wanaweza kurudi hapa, inanibidi kuondoka eneo hili”
“Usiku huu?”

“Yaaa usiku huu”
Mama Marim hakuwa na kitu cha kuzungumza ziidi ya kukubaliana na kile ambacho nilikuwa nimekikusudia, nikaanza kuvaa mwili wa plastiki unao nifanya niwe na muonekano wa mwamake, nilipo hakikisha nimemaliza kuvaa gauni langu, nikatoka nje nikiwa na funguo ya gari, nikafungua nyuma ya gari kwenye buti. Nikafungua begi la pesa, nikatoa kibunda kimoja cha dola kisha nikafunga na kurudi ndani.
“Chukua hizi pesa hakikisha unafungua biashara itakayo kusaidia maisha yako, sihitaji urudi kwenye hoteli kuendelea na ile kazi ya kuzalolishwa na watoto wadogo”
Mama Mariam akazitazama pesa zangu ninazo mpatia huku macho yakimtoka. Nikamshikisha pesa hizo mkinoni kisha nikachukua nguo zangu za kiume nilizo kuwa nimezivaa nikazikunja vizuri na kuzishika mkononi.
“Dany siamini kama ninaweza kupata pesa nyingi kiasi hicho”
“Ndio uamnini, mimi kwa sasa sina muda wa kuendelea kukaa hapa ninaondoka”

“Sawa Dany asante sana”
“Nitaendelea kumtafuta Marim sawa”
“Sawa Dany nashukuru”
Nikamiga busu la mdomo mama Marim, kisha nikabeba kila kilicho kuwa changu na kutoka nje, nikaingia kwenye gari langu na kuondoka. Japo ni usiku sikuwa na sehemu ya kueleka zaidi ya kutafuta sehemu nitakapo simamisha gari langu na kupumzika hadi itakapo timu asubuhi. Nikafika kwenye moja ya msitu maeneo ya Mbezi Temboni, nikasimamisha gari langu na kuzima taa kisha nikaikunjua siti yangu kidogo kisha nikalala.   
    Mtetemesho wa simu yangu niliyo iweka pembeni mwa siti ya gari, ndio ukanistua, nikafumbua macho yangu, nikaichukua kwa mkono wangu wa kushoto na kukuta ni mama ndio anaye nipigia.
“Shikamoo mama”
“Marahaba, sasa upo wapi?”
“Nipo kwenye moja ya msitu nimepumzika”
“Nina habari mbaya”
Ikanibidi kukaa vizuri kwenye siti yangu huku nikijiandaa kuisikiliza hiyo habari mbaya.

“Habari gani hiyo mama?”
“Kuna kikosi maalumu kutoka nchini Somalia leo, kimeingia kwa siri nchini Tanzania, na kina mpango wa kutekeleza tukio la kigaidi katika uwanja wa taifa wa mpira na mechi itakuwa ni Simba na Yanga”
Nikashusha pumzi kwa maana ni moja ya tukio ambalo sikuwa nalo kabisa katika mipango yangu
“Ila mama hiyo sio kazi yangu”
“Natambua sio kazi yako, ila tazama ni watu wangapi watakao poteza maisha yao pasipo kuwa na hatia na hichi wanacho kuja kukifanya leo ni ulipizaji kisasi kwa wezao walo uwawa kipindi kile kwenye dhiara ya raisi”
“Mungu wangu, sasa mama mimi nina anzia wapi?”
“Nakutumia picha za vijana hao watakao jitoa muhanga leo katika uwanja wa taifa. Wapo vijana wanne, ukiweza kuwatambua picha zao basi unaweza kufanikisha swala hilo la kuwaokoa maelfu ya watanzania”



from MPEKUZI

Comments