AISIIIII……….U KILL ME ( Sehemu ya 45 na 46 )

MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA                             
ILIPOISHIA 

“Mariamuuuuuuuuuuu”
Niliisikia sauti ya Mama Marim iliyo zidi kunichanganya na kujikuta nikikaa chini sakafuni huku machozi yakinilenga lenga. Nikanyanyuka taratibu na kumtazama Mariam, jinsi alivyo lala hajabadilisha hata mkao, mapigo yake ya moyo yamesimama kabisa jambo lililo zidi kunichanganya maradufu na saa yangu ya ukutani inaonyesha ni saa mbili kasoro usiku na muda si mrefu Babyanka atakuja kunipitia kwa ajili ya kwenda Marekani kuifanya kazi ya muheshimiwa riaisi.

ENDELEA
Mlango wa chumbani kwangu ukagongwa na kuyafanya maoigo yangu ya moyo kuzidi kwenda kasi kwa maana ninatambu atakuwa ni mama Mariam. Nnikashuka kitandani kwa haraka, nikafungua friji nikatoa chupa yenye maji ya baridi na kumwagia maji hayo Mariam usoni. Cha kumshukuru Mungu, akakurupuka huku akiwa anagema sana.
Nikawahi kumziba mdomo ili asiweze kupika kelele zitakazo sikika nje kwa maana mama yake amesha fika.
“Dany”
“Shiii”
“Mariammuuuu”
Tuliisikia sauti ya Mama Mariam akiita akiwa uwani na ttayari alisha ondoka mlangoni mwangu. Wasiwasi ukaanza kumjaa Mariam, akaanza kushuka kitandani huku akiwa anahema, akajaribu kupiga hatua mbili mbele ila nikagundua kwamba mwendo wake umebadilika na ana chechemea.
“Mungu wangu, Dany mama si atajua kwamba nimeutoa usichana wangu”

“Jikaze utembee vizuri, hatokustukia”
Nilizungumza huku nikimkalisha kwenye sofa taratibu. Tukatazama usoni, hapakuwa na aliye muongelesha mwenzake, hata sauti ya mama Mariam inayo ita ikawa haiendelei tena.
“Ngoja nitoke nikamzuge mama yako, hakikisha unafanya unatoka humu ndani asije kukustukia”
“Sawa”
Nikachukua taulo langu na kujifunga kiunoni mwangu,  nikachukua sabuni yangu na kutoka chumbani kwangu, kwenye kordo sikumkuta mtu wa iana yoyote. Nikaelekea kwenye mlango wa mbele ambapo nilihisi naweza kumkuta mama Marim, kwa bahati nzuri nikakutana naye mlangoni akiwa anaingia. Nikamshika mkono na kutoka naye nje.
“Vipi mbona unamwagikwa na jasho?”
“Nilikuwa ninafanya mazoezi, nikaoge kwa maana kuna sehemu nahitaji kuelekea”
“Unaeleka wapi tena honey”
“Ninakwenda nje ya nchi kikazi, kwahiyo sinto kuwepo Tanzania kwa siku kadhaa”
“Jamani Dany, hata kiu yangu hujaimaliza na wewe unataka kuondoka?”
“Imetokea kwa dharula tu, ndio maana nilipo isikia sauti yako nikatafuta ili niweze kukueleza juu ya hili mpenzi wangu”
“Na safari hiyo unaondoka saa ngapi?”

“Saa mbili hii ndio naondoka, hapa nimemaliza kufanya mazoezi na ninahitaji kueleka bafuni, nijiandae niondoke”
Mama Mariam akatazama kila sehemu ya eneo hili la nje tulipo kisha akanikumbatia na kuanza kuniyonya mdomo wangu. Tukalifanya tendo hilo kwa dakika kadhaa kisha tukaachiana.
“Nakuomb nikaoge”
“Sawa honey, ila Marim umemuona?”
“Nilimuona pale nilipo rudi na nikamuomba ufunguo, baada ya hapo sikufahamu ni sehemu gani aliyo elekea”
“Yaani huyu mtoto sijui atakuwa amekwenda wapi, ngoja nikamtazame hapo mbele kwa mama Jenifa”
“Sawa”
Mama Mariam akanipiga busu la mdomo kisha akatoka getini, alipo funga geti kwa haraka nikaingia ndani moja kwa moja nikaeleka chumbani kwangu, nikaufungua mlango na kuingia ndani. Sikumkuta Mariam, nikashusha pumzi na kuelekea chumbani kwake, nikamkuta akiwa amesimama katikati ya chumba huku amefunga kanga kifuani.
“Mama yako amekwenda kwa mama Jenifa, sasa fanya ukaoge kisha urudi ulale sawa?”
“Sawa”



from MPEKUZI

Comments