AISIIIII……….U KILL ME ( Sehemu ya 37 na 38 )

MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA
ILIPOISHIA   

“Umechukua kila kitu?”
“Ndio ila kuna hii karatasi hapa ina namba ya huyo bosi wao wa majambazi, pamoja na namba nyingine za wezake Jumaa.”
“Hembu nipatie”
Asma akanipatia karatasi hiyo iliyo kunjwa vizuri, nikaikunjua na kutazama namba za simu zilizo andikwa humo hususani namba ya huyo bosi wa Jumaa, sikuamini macho yangu kuikuta nama ya K2 ambayo ninaifahamu vizuri hata kama nikiwa sina simu. Nikahisi sio yenyewe labda nimekosea, nikamuomba simu Asma, akanikabidhi, nikajaribu kuingia katika upande wa kutuma pesa wa Tigo pesa, nikaiingiza namba hiyo ya simu na kiasi ninacho hitaji kutuma, yakatokea maandishi kutoka katika hudumu hii yanayo someka ‘Ingiza namba yako ya siri kutuma pesa kwa K2 kiasi ni shilingi elfu kumi’. Nikajihisi nguvu zikiniishia huku taratibu nikikaa kwenye sofa, huku mapigo ya moyo yakianza yakinienda kasi sana.

ENDELEA  
“Vipi Dany mbona umeogopa hivyo?”
“Hapana, nahitaji nikuondoe usiku huu huu”
“Mimi sina tatizo nakusikiliza wewe”
Sikuwa na haja ya kuingia bafuni na kuoga zaidi ya kuanza kuvaa nguo zangu kwa haraka sana, kitu ambacho ninahofia ni Asma kuziona bastola zangu jambo ambalo silihitaji alifahamu kwa muda huu. Nilipo maliza kufaa nguo, nikatoka nje ya nyumba yetu ikiwa tayari ni saa nne usiku. Nikaelekea kwenye sehemu wanapo egesha taksi za kukodi, nikamuita dereva mmoja nikaelekea naye hadi nyumbani. Nikaingia ndani huku nikiwa makini sana. Nikamkuta Asma akiwa amekaa kwenye sofa ananisubiria,

“Una baibui?”
“Ndio”
“Lipo karibu uweze kulivaa?”
“Ndio”
Haya litoe fasta fasta na ulivae”
Asma akafanya kama nilivyo mueleza, begi lake la nguo nikaliweka kitandani, nikalifungua kwa haraka, akaanza kuchambua nguo huku akitafuta basibui lake, alipo liona, akavua dera lake kwa haraka, na kuanza kuvaa baibui lake hilo lenye kitambaa kinacho ificha sura yake. Nikamsaidia kurudisha nguo zake kwenye begi haraka haraka kisha nikachungulia kwenye kordo sikuona mtu, tukatoka huku nikifunga chumba changu na kuanza kutembea kwa mwendo wa umakini sana huku macho yangu yote yakiwa mbele na Asma akinifwata kwa nyuma. Tukafanikiwa kutoka nje kabisa ya nyumba pasipo kuonekana na mtu anaye tufahamu ila Asma ni ngumu zaidi kufahamika kwani sura yake ameificha kwa kitambaa hicho cha baibui kilicho mbakisha macho wazi.

Tukaingia kwenye taksi, nikaanza kumpa dereva maelekezo ya wapi atupeleke. Safari ikaanza huku muda wote Asma akiwa amenishika mkono wangu wa kulia, akiwa na wasiwasi mwingi sana usoni mwake. Tukafika katika hoteli ya MK, iliyopo kwenye eneo la Mbezi Beach. Nikawa wa kwanza kushuka kwneye taksi na kumuacha Asma ndani ya taksi, nikaeleka hadi mapokezi, nikalipia chumba kimoja cha gorofani kisha nikarudi kwenye taksi.
“Ngoja nikusaidie begi”
Nilizungumza huku nikilishika begi la Asma.
“Kaka haujanilipa bado”
“Ohoo sorry ndugu yani nimejisahau bei gani?”
“Elfu ishirini na tano”
Nikanipapasa kwenye waleti yangu na kukuta shilingi elfu kumi, jambo lililo anza kunipa wasiwasi, kwani hoteli niliweza kulipia kwa kadi ya malipo ambayo ninatembea nayo popote niendapo.
“Vipi?”
“Nimepungukiwa elfu kumi na tano”
“Ngoja”
Asma akafungua kipochi chake na kutoa shilingi elfu shirini na tano na kumkabidhi dereva huyo aliye tuaga na kuondoka. Tukaeleka ndani ya hoteli, tukaingia kwenye lifti na kuelekea gorofa ya tano. Tukaingia kwenye chumba nilicho kikodisha. Nikafunga kwa ndani na Asma akaanza kuvua baibui lake kisha akanirukia na kunikumbatia kwa nguvu huku machozi yakimwagika usoni mwake.
“Ohoooo Dany nakuomba usije ukaniacha, nimefanya haya yote kwa ajili yako”

“Siwezi kukuacha Asma, natambua ni kipindi gani ambacho unapitia, ninakuahidi nitakulinda katika maisha yangu yote”
Nilizungumza kwa hisia kali na kumfanya Asma azidi kunikumbatia kwa furaha na hisia nzito, tukaachiana na kuanza kunyonyana midomo yetu safari hii, kila mmoja akajiachia na kuwa huru kwa mwenzake kwa maana tumesha jihalalisha mioyoni mwetu kuwa wapenzi. Kusema kweli Asma ni mzuri na ana vigezo vyote vya kuwa mwanamke wa ndoa.
Akaanza kunivua nguo na kubaki kama nilivyo zaliwa. Tukaingia kwneye mzunguko mwengine wa kupeana raha na burudani. Haikuwa mechi kama ya kwanza ila hii ikawa ni zaidi ya mechi ya kwanza. Tukapeana utamu halisi wa mume wa mke huk u kila mmoja akiwa anamwaga sifa kwa mwenzake, tukamaliza kwa wakati mmoja huku kila mmoja akiwa na furaha kubwa moyoni mwake.



from MPEKUZI

Comments