TANGA RAHA- Sehemu ya Nane ( 8 )

MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA
ILIPOISHIA
Simu yangu ikaanza kuita nikapiga hatua za haraka kwenda kuipokea huku nikimgonga kidogo muhudumu begani kitendo cha kuinama na kuiokota suruali yangu iliyopo chini ili kuitoa simu yangu mfukoni gafla taulo langu likafunguka na kudondoka chini huku muhudumu akibaki ananishangaa.

ENDELEA
  Nikashika na bumbuwazi huku nisijue ni nini nifanye huku muhudumu akiwa hakwepeshi hata jicho katika kunitazama katika kiko yangu.Nikaitoa simu na kukuta ni Rahma anaye piga.Nikaipokea huku nikiwa ninaliokota taulo taratibu
“Baby umeshaletewa chakula”
“Ndio baby”
“Ok mimi nimeshafika kwa bibi nikitaka kuja huko nitakuambia”
“Sawa mke wangu”
Nikakata simu na kumkuta muhudumu akiwa anmenata kama amedandishwa na superglue kwani hakutingishika wala kukwepesha sura yake katika taulo ambalo limeifunika koki yangu
“Hei dada…..dada”

    Akastuka na kwa aibu akatoka pasipo kuzungumza chochote na akaufunga mlango na nikabaki nikijifikiria ni kitu gani cha ajabu alicho kiona muhudumu mpaka akawa anashangaa kiasi cha kunifanya nimshangae.Nikala chakula ambacho kimeletwa na muhudumu kwenye chumba changu.Nikamaliza na kuvaa nguo zangu na kwenda kutembelea maeneo ya hteli hiyo yenye mandhari mazuri ya kupendeza.

Nikatafuta sehemu ya kukaa iliyopo kandokando ya swimming pool na kagizia juisi baridi na kuanza kunywa huku nikimsubiri Rahma kuja kunihukua.Nikiwa ninaendelea kunywa juisi yangu kuna wasichana wawili warembo wakaja kukaa kwenye kitanda kilichopo pembeni yangu huku wakianza kuvua nguo zao kwa ajili ya kuogelea katika swimming pool hilo

    Wakabaki na nguo zao za ndani na kujitosa ndani ya maji na kuanza kuogelea.Wakiwa wanaendelea kuogelea mmoja anayeonekana si mzoefu sana katika kuogelea akaanza kupiga kelele ya kuomba msaada wa kuokolewa.Nikanyanyuka haraka haraka na kuvua viatu na kuitoa wallet yangu yenye pesa pamoja na simu mfukoni na kujitosa ndani ya maji.Nikaogelea hadi katika eneo alilo kuwepo nikamsubiria maji ya mlegeze kwanza kwa sekunde kadhaa nikihofia enedapo nikimuokoa akiwa katika hali yake ya kuwa na nguvu anaweza kunizamisha na mbaya zaidi sehemu waliyopo katika swimming pool hilo kuna kina kirefu kwenda chini.

Nikamshika vizuri na kwenda naye njee na kumlaza katika ukingo wa swimming pool hilo huku nikianza kumminya minya kifuani ili atapike maji aliyo yanywa nikaanza kumpa pumzi kwa kumpulizia mdomoni kwake.Wahudumu wa kiume wa hotel wakawa tayari wameshafika katika eneo hilo na kunisaidia katika zoezi la kumtapisha msichana huyo huku mwenzake akiwa pembeni akilia

==>Endelea Nayo <<kwa Kubofya Hapa>>


from MPEKUZI

Comments