SORRY MADAM -Sehemu ya 98 & 99 (Destination of my enemies

MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA
ILIPOISHIA

   Kila mtu moyo wake ulizidi kumuenda mbio akiwa ndani ya gari hilo. Madam Mery taratibu akajikuta akianza kusali sala yake ya mwisho kwa maana wanapo elekea kifo kipo mbele yao.
“Fanya uwashe gari”
Manka alizungumza huku machozi yakianza kumwagika, kila jinsi dereva alivyo jaribu kuwasha gari lake, halikuwaka hadi ikafika kipindi akakata tama kabisa. Matairi ya mbele tayari yalisha anza kuelea hewani kwenye korogo hilo linalo endelea kulika taratibu taratibu na matairi ya nyuma pekee ndio yapo kwenye ardhi.
“Ohoo Mungu wangu tunakufa”
Manka alizungumza huku akiyafumba macho yake, akisubiria gari hiyo kuangukia kwenye korongo hilo na huo ndio utakuwa ni mwisho wa maisha yao.

ENDELEA
       Wakiwa katika hali ya sinto fahamu, gafla wakastukia watu wawili wa kiwa nyima yao wakijitahidi kulishika gari hilo kwa nyuma. Walipo geuka wakawaona Shamsa na Eddy ambaye Manka anamtambua kwa jina la Ericksom. Kwa ishara Shamsa akawa anawaomba wateremke.
Madam Mery akawajibu kwa vitendo kwamba hawawezi kushuka kutokana milango imejifunga na hakuna kitu chochote kinacho weza kufanya kazi ndani ya gari hilo.
“Tunafanyaje sasa Eddy?”
“Tafuta jiwe uvunje kioo”
“Sawa”
Shamsa akaanza kutafuta jiwe ambalo linaweza kupasua kioo cha gari hilo, kwa bajati nzuri akapata jiwe moja kubwa, kwa haraka akarudi nalo hadi sehemu ilipo gari.
“Vunja kioo kimoja wapo”

Eddy alizungumza huku jasho likimwagika, kwa maana shuhuli ya kuizuia gari hilo lisitumbukie kwenye korongo hilo ni kubwa sana kwake. Kila Shamsa alivyo jaribu kupasua kioo cha upande alio kaa madam Mery, hakikupasuka wala kuonyesha dalili ya mpasuko.
“Mungu wangu gari hii ni bullet proff na haaingia risasi, ndio maana kioo chake hakipasuki.”
Shamsa alizungumza huku machozi yakimlenga lenga, kwa maana juhudi anazo zifanya zimekuwa ni bura kabisa. Gafla taa za nyuma ya gafi hizo zikaanza kuwaka, dereva kwa haraka akajaribu kuminya kitufe cha kufungua milango hiyo akafanikiwa. Manka akajirusha nje, madam naye akafanya hiyo hivyo, shuhuli ikawa kwa dereva ambaye amekaa siti ya mbele kabisa. Uzito ulizidi kuongezeka pale alipo kuwa kwenye harakati za kutaka kuhamia siti ya nyuma ili atoke kwa maana milango yote ya mbele endapo ataifungua na kujaribu kutoka basi safari yake ni moja kwa moja hadi kwenye korongo hilo.

“Nisa…..iidi…..eeeni”
Eddy alizungumza huku akijikaza kadhi ra uwezo wake kuhakikisha kwamba analizuia gari hilo lililo anza kusogea mbele taratibu likelekea kudumbukia kwenye korongo hilo.
Wote watatu wakaanza kulishika gari hilo kwa nyuma sehemu ambapo Eddy amepashika. Dereva huyo ambaye alisha anza kukinusa kifo kwa haraka haraka akajirusha siti ya nyuma na kujirusha nje. Kitendo cha yeye kutoka Eddy na wezake wakaliachia gari hilo na likadumbukia kwenye korongo hilo refu kwenda chini.
“Ohooo honey”
Manka alizungumza huku akimkumbatia Eddy kwa nguvu. Shamsa akataka kuwaachanisha ila madam Mery akamshika mkono na kutingisha kichwa akimuashiria kwamba asifanye chochote. Askar wengine kutoka ikulu nao wakafika eneo hilo wakiwa na bunduki zao mikononi. Shamsa alipo waona askari hao akataka kuondoka ila askari mmoja akamshika bega.

“Subiri mwaya”
Kumbe sababu ya askari huyo kumshika Shamsa bega ni kutokana na Manka kumuonyeshea askari huyo kwa ishara amzuie asiondoke eneo hilo. Manka akaachiana na Eddy na kumfwata Shamsa pale alipo simama.
“Asante kwa kuyasaidia maisha yetu”
“Usijali ni kitu cha kawaida”
Manka akampa mkono Shamsa, aliye upokea taratibu. Wakaachiana mikono huku Manka akionekana kumtazama Shamsa usoni. Kumbukumbu zake zikarejea hadi pale hospitalini, alipo weza kumuona Shamsa akiwaangusha walinzi wawili walio pewa kazi ya kumlinda akiwa na Erickson ndani. Kumbukumbu zake hazikuishia hapo akakumbuka jinsi walivyo pambana ndani ya chumba hicho ili asichukuliwe Erickson ila walipo ingia Madam Mery na binti mwengine wa Kijapani hapo ndipo walipo mzidi nguvu na kuondoka naye.

“Weeee……..”
Manka hadi anastuka kutoka kwenye dimbwi la mawzo, tayari Shamsa alisha ondoka eneo hiloakijichanganya watu wanao shangaa shangaa kilicho tokea.
“Mtafuteni yule binti sasa hivi”
Manka alitoa amri kwa askari wake kutoka ikulu ambao walianza kutawanyika kumfwatilia ni wapi Shamsa alipo elekea huku wengine wanne wakibakia katika eneo hilo wakiimarisha ulinzi dhidi yake.
Eddy na Madam Mery walibaki kukonyezana kwa maana waliweza kumshuhudia Shamaa akiondoka eneo hilo baada ya Eddy kumpa ishara ya kukimbia huku akimkabidhi funguo za gari la dokta pasipo mlinzi au mtu mwengine yoyote kuweza kuona tukio hilo.

“Erickson…….!!!”
Manka alimuita Eddy huku akiwa amemkazia macho na kumtazama kwenye upande wa kushoto wa koti jeupe alilo livaa.
“Nini?”
Eddy aliuliza huku akiteremsha macho yake kuangalia ni kitu gani kinacho endelea. Eddy macho yakamtoka, wasiwasi ukamjaa mwingi, hii ni baada ya kuona damu nyingi ikiwa imelowanisha koti hilo alilo vaa ikiashiria kwamba mshono wake umepata tatizo ambalo ni kubwa sana. Kwa haraka walinzi wa Manka wakamchukua Eddy huku wakimsaidia kushika pande zote mbili za mikono yake na kuondoka naye hadi kwenye magari yao yalipo huku Manka na Madam Mery wakimfwata kwa nyuma.
“Madam tumpeleke hospitali gani?”
Dereva alizungumza huku wakiwa wote tayari wamesha ingia kwenye gari hilo.
“Wewe twende tu”
Manka alizungumza huku machozi yakimwagika usoni mwake kila alipo mtazama Erickson wake aliye laza kichwa mapajani mwake na kujikausha kimya asizungumze chochote
                                                                                                            ***
“Mkuu hatujaweza kumpata kiongozi na hali iliyo jitokeza huku naamni kwa sama ninaamini muna ishuhudia kwneye televishion”

Mmoja wa vijana wa kikosi maalumu kutoka D.F.E walio tumwa kuweza kumuokoa mzee Godwin alizungumza na simu akiwasiliana na John ambaye yupo kwenye ukumbi wa kutano Serena Hotel akiwa na viongozi wengine wakisuribia kuweza kupata matokeo mazuri kama mzee Godwin amapatikana au laa.
“Ondokeni eneo hilo, na sura zenu zisionekane kwenye televishion”
“Sawa mkuu”
Kijana huyo akakata simu, kwa haraka akelekea kwenye uapende wa pili wa barabara, alipo waacha wezake ndani ya gari, wakiwa wamenuusurika kudumbukia kwenye korongo hilo lisa moja lililo kwisha kupita.
“Vipi wamesemaje?”
“Wamesema tuondoke sura zetu zisionekane eneo hili wala kwenye televishion”
“Poa”
Dereva akawasha gari na wakaondoka eneo hilo. Mmoja wao aliye kaa siti ya mbele pembeni ya dereva akashusha pumzi kisha akaanza kuzungumza.

“Jamani hivi munajua laiti tungesubutu kukomaa na wale makachero wa kwanza kuingia ndani mule ya msitu na sisi habari yetu ingekuwa imesha kichwa?”
“Kweli mwanagu, kwa maana tangu nizaliwe sijawahi kuona bomu la namna hii”
“Yaani muda ule nilipo anza kuuona ule mpasuko wa ardhi, akili yangu ilinituma kwa haraka kurudisha gari nyuma hadi tukafika barabarani”
“Nasikia waseng** wote walio kuwemo ndani ya msitu wamedanja”
“Weee kwa timbwili lile unahisi wasinge danja”
“Alafu kumbe mtoto wa mzee alikuwepo”
“Nani?”
“Manka, naye angeenda na maji”
“Aisee tuache utani ila lile toto ni lizuri”
“Anaye lila lile naamini kwamba ana faidi ile mbaya”
“Kweli, ukishikilia ile mitako na mihispi, mamayeee”
“Acheni ujinga nyinyi tufikirie ni jinsi gani tunaweza kumpata mzee”
Mkuu wao alizungumza na kuyakatisha mazungumzo ya vijana wake ambao wote wanamezea mate Manka mtoto wa bosi wao ambaye ni Mzee Godwin.



from MPEKUZI

Comments