Mahakama yaamuru ‘Nabii Tito’ akapimwe Mirembe.....Kesi Imeahirishwa hadi Machi 5

Mahakama ya Wilaya ya Dodoma imemuamuru mkuu wa Gereza la Isanga kumpeleka katika taasisi ya magonjwa ya akili mshtakiwa Onesmo Machibya maarufu Nabii Tito, ili kujua iwapo ana akili timamu au la.

Hakimu mkazi mfawidhi wa mahakama hiyo, James Karayemaha ametoa agizo hilo leo Jumatatu Februari 19,2018.

Amesema Magereza wanachelewesha haki ya mshtakiwa na kwamba, anashangaa ni kwa nini wanashindwa kutekeleza agizo la kumpeleka kufanyiwa uchunguzi.

"Naagiza amri ya Mahakama itekelezwe, apelekwe taasisi ya magonjwa ya akili Isanga (Mirembe) si kama alivyoleta vielelezo kutoka Muhimbili," amesema Karayemaha.

Hakimu ameahirisha kesi hadi Machi 5,2018 itakapotajwa kwa ajili ya kupokea taarifa ya uchunguzi.


from MPEKUZI

Comments