Mgombea Wa Ubunge Chadema Arudisha Fomu

Mgombea Ubunge wa Jimbo la Kinondoni kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Salum Mwalimu, leo Januari 20, 2017 amerudisha fomu za kuwania kinyang’anyiro hicho katika ofisi ya Msimamizi wa Uchaguzi, Manispaa ya Kinondoni Jijini Dar es Salaam.

Katika Uchaguzi huo, Mwalimu atachuana na aliyekuwa Mbunge wa Kinondoni kupitia Chama Cha Wananchi (CUF), Maulid Mtulia kabla ya kujivua uanachama na kuhamia CCM ambapo ameteuliwa tena na chama chake kupeperusha bendera.


from MPEKUZI

Comments